Hakuna uchunguzi wa kisayansi ambao umeonyesha faida
yoyote inayopatikana kwa kuua Albino.
Madai ya kuwepo kwa faida katika mauaji ya Albino ni uvumi
mtupu unaoimarishwa na imani ya kishirikina na hazina msingi.
Kwa bahati mbaya uvumi huu umeimarika katika baadhi ya
jamii na hivyo kupelekea Albino kupata madhara makubwa
ya kujeruhiwa na wakati mwingine kuuawa katika jitihada za
kupata damu au viungo vya miili yao.
Kuua na kujeruhi ni kosa la jinai linaloadhibiwa kisheria. Serikali
kwa sasa ina msimamo mkali wa kukomesha makosa haya ya jinai
kwa kutumia sheria kuhukumu watuhumiwa wanapokamatwa hii
ni pamoja na kuelimisha jamii.
Watu wanaoua Albino wanapata faida gani?






Discussion
Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.
You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.
Log in to participate