Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu,; anza Novena kwa Moyo Mtk wa Yesu katika Alhamisi ya Sikukuu ya Ekaristi Takatifu (Corpus Christi), yaani Alhamisi ya wiki moja kabla ya Sikukuu ya Moyo Mtk (au Alhamisi baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk). Endapo Sikukuu hii itaadhimishwa siku ya Dominika inayofuata Sikukuu yenyewe kama inavyofanyika mahali pengi, basi novena inatakiwa ianze Ijumaa ya baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk ili imalizike Jumamosi kabla ya Dominika ya sikukuu hii ya Moyo Mtk kwa Yesu.

WIMBO:

YESU KRISTU TWASIFU MOYO WAKO
Yesu Kristu, twasifu Moyo wako, sisi sote, milele mali yako
Tunakupa, nyoyo zote zetu, Mukombozi, Mfalme Mungu wetu;
Tunakupa, nyoyo zote zetu, Mukombozi, Mfalme Mungu wetu!

Watu wengi, wanakaa ugenini, wazunguka, wenye ukiwa chini,
Uwatie huruma yako kuu, roho zao, uziinue juu;
Uwatie huruma yako kuu, roho zao, uziinue juu!

Uwe Mfalme, wa wale washikwao, na ushenzi, na ukaidi wao
Wapelekee ufalme wa Mungu, ni Mchunga mmoja Zizi moja tu;
Wapelekee ufalme wa Mungu, ni Mchunga mmoja Zizi moja tu!

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi, basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi wkako. Amina.

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.
Kwenye Msalaba Sali:

โ€œEe Yesu tupe moyo wako kama amana ya upendo wako na kimbilio letu, ili tupate pumziko salama wakati wa maisha yetu na faraja tamu saa ya kufa kwetuโ€.
Baba Yetu โ€ฆโ€ฆ..
Salamu Maria โ€ฆโ€ฆ. (mara tatu)
Nasadiki โ€ฆโ€ฆโ€ฆ..

Kwenye chembe kubwa Sali (Badala ya โ€˜Baba Yetuโ€™):
โ€œNinakuabudu, ninakutukuza na ninakupenda, Ee Moyo wa Yesu wangu mpenzi, uliopenywa na huzuni nyingi kwa ajili ya dhambi, ambazo zimekuwa zikitendwa hata leo, dhidi ya Sakramenti Takatifu sana ya Altare. Ninakutolea hapo kwa kuridhika, moyo wa Mama yako mpendevu, na mastahili ya watakatifu. Aminaโ€.

Kwenye chembe ndogo sali (Badala ya โ€˜Salamu Mariaโ€™):
โ€œEe Moyo Mtakatifu wa Yesu, uwakao mapendo kwetu, washa nyoyo zetu kwa mapendo yako"

LITANIA YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie Kristo utusikilize
Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia Mungu Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja Utuhurumie
Moyo wa Yesu Mwana wa Baba wa Milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu uliotungwa na Roho Mtakatifu mwilini mwa Mama Bikira Maria Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulioungana na Neno wa Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulio na utukufu pasipo mfano Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hekalu takatifu la Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hema la Yule aliye juu Utuhurumie
Moyo wa Yesu tanuru lenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, nyumba ya Mungu na mlango wa Mbingu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tanuru yenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chombo cha haki na upendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaojaa upendo na wema Utuhurumie
Moyo wa Yesu, kilindi cha fadhila zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaostahili sifa zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaotawala mioyo yote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, zinamokaa hazina za hekima na elimu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliopendelewa na Mungu Baba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotuenezea maziada yake Utuhurumie
Moyo wa Yesu, mtamaniwa wa vilima vya milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu, wenye uvumilivu na huruma nyingi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tajiri kwa wote wenye kukuomba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya uzima na utakatifu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, malipo kwa dhambi zetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, ulioshibishwa matusi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliovunjika kwa sababu ya ubaya wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotii mpaka kufa Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliochomwa kwa mkuki Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya faraja zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uzima na ufufuo wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, amani na upatanisho wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sadaka ya wakosefu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unamokaa wokovu wao wenye kukutumaini Utuhurumie
Moyo wa Yesu, matumaini yao wenye kuzimia kwako Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sababu ya furaha ya watakatifu wote Utuhurumie
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusamehe Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusikilize Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie

Kiongozi: Yesu mwenye Moyo mpole na mnyenyekevu,
Wote: Ufanye mioyo yetu ifanane na Moyo wako

TUOMBE:ย (W) Ee Mungu Mwenyezi milele, uuangalie Moyo wa mwanao mpendelevu, pia na heshima na malipo aliyokutolea kwa ajili ya wenye dhambi, uridhike, uwaondolee wenye kuomba toba kwako kwa njia ya huyo Mwanao Yesu Kristo anayeishi na kutawala nawe pamoja na Roho Mtakatifu, Mungu milele. Amina.

P.S. Mwezi wa sita ni wa kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu. Vitu vya kufanya ni pamoja na kushiriki Misa takatifu kila siku, kumtembelea Bwana Yesu katika Ekaristia, kusali Rozari ya Moyo Mtakatifu wa Yesu kila siku, kusali Litania za Moyo Mtakatifu wa Yesu, kuimba nyimbo za kuusifu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na kadhalika. Kwa kufanya hayo na mengineyo yanayofanana nayo, waumini hujichotea Baraka na neema nyingi za kimwili na kiroho.

SALA YA NOVENA

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema โ€œKweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwaโ€, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba โ€ฆโ€ฆ.. (Taja ombi lako)
Baba Yetuโ€ฆ.., Salamu Maria โ€ฆโ€ฆ.., Atukuzwe Babaโ€ฆโ€ฆ..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema โ€œKweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewaโ€, tazama kwa jina lako ninaomba โ€ฆโ€ฆ. (Taja ombi lako)
Baba Yetuโ€ฆ.., Salamu Maria โ€ฆโ€ฆ.., Atukuzwe Babaโ€ฆโ€ฆ..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema โ€œKweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamweโ€, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba โ€ฆโ€ฆ.. (Taja ombi lako)
Baba Yetuโ€ฆ.., Salamu Maria โ€ฆโ€ฆ.., Atukuzwe Babaโ€ฆโ€ฆ..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali โ€˜Salamu Malkiaโ€™ na kuongezea, โ€˜Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombeeโ€™.

P.S. โ€“ Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

SALA YA MAOMBI

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe tegemeo langu na tumaini langu dhabiti. Ndiwe mwenye dawa ya maovu yangu yote, malipizi ya makosa yangu yote. Waweza kunipatia haja zangu na neema ninazoziomba mimi na wengine. Wewe uko ili kutusaidia sote, ndiwe mwanga mkuu usiozimika, ndiwe chanzo cha nguvu, uvumilivu, amani na faraja. Nina hakika kuwa maombi yangu hayatakuchosha, nawe hutaacha kunisaidia, kunilinda, kunipenda, kwani, ee Moyo Mtakatifu , upendo wako hauna mwisho. Ee Moyo Mtakatifu, unihurumie, kwa ajili ya maombi yangu, kadiri ya huruma yako. Nawe katika sisi, na kwa ajili yetu, ufanye lolote unalolihitaji, kwani tunajitoa kwako kwa imani na uhakika thabiti kwamba kamwe hautatuacha, kwa milele. Amina.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Anna Malela Guest Jun 14, 2024
๐Ÿ™โœจโค๏ธ Neema za Mungu zikufunike
๐Ÿ‘ฅ Edwin Ndambuki Guest Jan 1, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Dec 22, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Anna Sumari Guest Nov 20, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Miriam Mchome Guest Nov 13, 2023
๐Ÿ™โค๏ธโœจ Asante Mungu kwa kila kitu
๐Ÿ‘ฅ Anna Sumari Guest Oct 14, 2023
๐Ÿ™โœจ Mungu atakuinua
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest Aug 4, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ John Malisa Guest Jul 10, 2023
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mushi Guest Jun 23, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Jun 5, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Jun 3, 2023
๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Rose Mwinuka Guest May 21, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Mar 23, 2023
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Moses Mwita Guest Feb 16, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Dec 30, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Kenneth Murithi Guest Nov 15, 2022
๐Ÿ™โค๏ธ๐Ÿ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Nov 13, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Stephen Amollo Guest Oct 22, 2022
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Elijah Mutua Guest Oct 20, 2022
๐Ÿ™๐Ÿ’– Mungu wetu asifiwe
๐Ÿ‘ฅ Jackson Makori Guest Aug 4, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Jul 1, 2022
๐Ÿ™๐ŸŒŸโค๏ธ Nakuombea heri
๐Ÿ‘ฅ Raphael Okoth Guest Jun 26, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Charles Wafula Guest Jun 25, 2022
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Jun 8, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Samuel Were Guest May 24, 2022
๐Ÿ™โœจ Mungu asikie maombi yetu
๐Ÿ‘ฅ Samuel Omondi Guest Feb 4, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Miriam Mchome Guest Jan 23, 2022
๐Ÿ™๐Ÿ’– Asante kwa neema zako Mungu
๐Ÿ‘ฅ Mariam Hassan Guest Oct 15, 2021
๐Ÿ™โค๏ธ Mungu ni mlinzi wetu
๐Ÿ‘ฅ Michael Onyango Guest Oct 4, 2021
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Aug 28, 2021
Amina
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest Jun 21, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Kenneth Murithi Guest Dec 1, 2020
๐Ÿ™๐Ÿ’–โœจ Neema yako ni ya kutosha
๐Ÿ‘ฅ Isaac Kiptoo Guest Nov 25, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Joyce Nkya Guest Oct 2, 2020
๐Ÿ™โค๏ธโœจ Mungu akujalie furaha
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest Oct 2, 2020
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Jul 28, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Betty Akinyi Guest Jun 28, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest May 23, 2020
๐Ÿ™๐ŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest Apr 3, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Feb 16, 2020
๐Ÿ™๐ŸŒŸ Mbarikiwe sana
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Jan 14, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Mary Njeri Guest Jan 4, 2020
๐Ÿ™โค๏ธ Mungu akubariki
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Dec 23, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Kevin Maina Guest Dec 22, 2019
๐Ÿ™๐Ÿ’–๐Ÿ™ Mungu akufunike na upendo
๐Ÿ‘ฅ Esther Nyambura Guest Dec 12, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Aug 6, 2019
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Diana Mallya Guest Jul 11, 2019
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Stephen Mushi Guest May 25, 2019
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mutheu Guest Feb 17, 2019
๐Ÿ™๐ŸŒŸ Mungu akujalie amani
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Dec 21, 2018
๐Ÿ™๐Ÿ’– Nakusihi Mungu
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Dec 5, 2018
๐Ÿ™๐ŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Nov 7, 2018
๐Ÿ™โค๏ธ๐Ÿ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
๐Ÿ‘ฅ Grace Mushi Guest Oct 23, 2018
๐Ÿ™โค๏ธ Mungu ni mkombozi
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kangethe Guest Oct 4, 2018
๐Ÿ™โค๏ธ๐Ÿ’– Bwana akujalie baraka
๐Ÿ‘ฅ Chris Okello Guest Aug 30, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Grace Njuguna Guest Aug 13, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mahiga Guest Jul 14, 2018
๐Ÿ™โœจ๐Ÿ’– Mungu atajibu maombi yako
๐Ÿ‘ฅ Charles Mboje Guest Jun 23, 2018
๐Ÿ™โค๏ธ Mungu ni mwaminifu
๐Ÿ‘ฅ Peter Mugendi Guest May 4, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Apr 26, 2018
Endelea kuwa na imani!

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About