MAHITAJI
Unga - 2 Vikombe
Sukari ya icing - 1 Kikombe
Siagi - 250 gm
Yai - 1
Vanilla - 2 Vijiko vya chai
Baking powder -1 Kijiko cha chai
Jam - ยผ kikombe
Lozi - ยผ kikombe
JINSI YA KUPIKA
Koroga siagi na sukari katika mashine ya keki (cake mixer) mpaka iwe laini (creamy).
Tia yai na vanilla koroga mpaka mchanganyiko uwe laini kama sufi.
Tia unga na baking powder changanya na mwiko.
Chota mchanganyiko kwa mkono (kiasi cha kijiko kimoja cha supufanya duara kisha weka kwenye treya ya kupikia.
Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam na tupia lozi zilizomenywa na kukatwa katwa.
Pika (bake) katika oven moto wa 375ยฐ F kama muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama
No comments yet. Be the first to share your thoughts!