MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
- Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
- Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
- Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
- Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
- Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
- Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
- Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
- Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
- Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
- Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
- Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
- Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
- Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
- Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
- Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
- Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
- Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
- Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
- Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuungβarisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
- Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
Karibu Vitatabu vya Kikatoliki
[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
Monica Adhiambo (Guest) on July 24, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Anna Malela (Guest) on July 16, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Grace Majaliwa (Guest) on July 15, 2017
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Joseph Kitine (Guest) on July 4, 2017
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Diana Mallya (Guest) on June 7, 2017
ππ Asante kwa neema zako Mungu
John Lissu (Guest) on January 18, 2017
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Rose Lowassa (Guest) on December 28, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mercy Atieno (Guest) on December 15, 2016
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Nicholas Wanjohi (Guest) on November 16, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Patrick Mutua (Guest) on September 7, 2016
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Henry Sokoine (Guest) on June 11, 2016
πππ« Mungu ni mwema
Francis Mrope (Guest) on March 14, 2016
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Bernard Oduor (Guest) on February 5, 2016
Dumu katika Bwana.
Grace Majaliwa (Guest) on February 3, 2016
Rehema zake hudumu milele
Elijah Mutua (Guest) on December 25, 2015
πβ€οΈ Mungu akubariki
John Mwangi (Guest) on November 25, 2015
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Thomas Mwakalindile (Guest) on November 19, 2015
Mungu akubariki!
Frank Macha (Guest) on September 17, 2015
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Alex Nakitare (Guest) on September 8, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Ann Wambui (Guest) on September 4, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Nora Kidata (Guest) on July 13, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
Elijah Mutua (Guest) on July 8, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Alice Mwikali (Guest) on May 15, 2015
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Joyce Mussa (Guest) on May 12, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima