Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)

  1. Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
  2. Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
  3. Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
  4. Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
  5. Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.

MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)

  1. Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
  2. Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
  3. Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
  4. Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
  5. Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.

MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)

  1. Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
  2. Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
  3. Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
  4. Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
  5. Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.

MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)

  1. Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
  2. Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
  3. Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
  4. Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
  5. Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

Karibu Vitatabu vya Kikatoliki

[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 84

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Jul 24, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Jul 16, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Jul 15, 2017
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Jul 4, 2017
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Jun 7, 2017
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jan 18, 2017
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Dec 28, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Dec 15, 2016
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Nov 16, 2016
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Sep 7, 2016
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Jun 11, 2016
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Mar 14, 2016
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Feb 5, 2016
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Feb 3, 2016
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Dec 25, 2015
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Nov 25, 2015
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Nov 19, 2015
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Sep 17, 2015
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Sep 8, 2015
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Ann Wambui Guest Sep 4, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jul 13, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Jul 8, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest May 15, 2015
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest May 12, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About