Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate wa kidunia/ ukafanya mwujiza na kuugeuza/ kuwa Mwili wako azizi./ Kwa mapendo ukawapa Mitume Mwili huo/ uwe kumbukumbu la mateso yako mastahivu./ Uliwaosha miguu kwa Mikono yako Mitakatifu./

Uheshimiwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Kwa kuhofu mateso na kifo,/ Mwili wako usio na kosa ulitoka jasho la damu/ badala ya maji./ Juu ya hayo uliutimiza wokovu wetu/ uliokuwa umetaka kuufanya./ Hivyo ulionyesha waziwazi mapendo yako/ uliyo nayo kwa wanadamu./

Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipelekwa kwa Kayafa,/ Wewe uliye Hakimu wa wote./ Ukaruhusu kwa unyenyekevu kutolewa kwa Pilato/ uhukumiwe naye./

Utukufu uwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa ulivumilia kuchekwa tena/ uliposimama huko,/ umevaa joho jekundu,/ umetiwa taji ya miiba mikali sana Kichwani,/ ukavumilia kwa saburi kubwa/ kutemewa mate katika Uso wako mzuri,/ kufumbwa Macho,/ na kupigwa mno na wajeuri/ ngumi na makofi Mashavuni na Shingoni./

Sifa iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ Kwa uvumilivu mkubwa ulikubali kufungwa nguzoni,/ kupigwa mijeledi kijeuri,/ kujaa damu na hivyo kusukumwa barazani kwa Pilato./ Ulionekana kama mwanakondoo asiye na kosa./

Heshima iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umehukumiwa Mwili wako mzima/ Mtukufu wenye kutoka damu/ ufe msalabani./ Ulichukua msalaba kwa Mabega yako Matakatifu/ na kuumwa sana./ Kwa ghadhabu walikusukuma mbele/ mpaka mahali pa mateso,/ wakakunyang’anya nguo zako./ Hivyo ulikubali kupigiliwa msalabani./

Heshima ya milele upate Wewe,/ Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa katika taabu kubwa hii,/ ulimkazia Mama yako mstahivu/ Macho yako ya hisani na mapendo/ na unyenyekevu,/ ndiye Mama yako asiyekosa hata mara moja/ wala kukubali dhambi yeyote./ Ulimweka katika ulinzi mwaminifu/ wa Mfuasi wako ili kumtuliza./

Milele utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa mwenyewe taabani,/ uliwapa wakosefu wote/ matumaini ya kuondolewa dhambi/ kwa kumwahidia mnyang’anyi aliyekuendea/ utukufu wa paradisi kwa huruma yako./

Sifa ya milele iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kila saa ulipovumilia uchungu/ na taabu kubwa mno msalabani kwa ajili yetu sisi wakosefu,/ maumivu makali sana/ yaliyotoka katika majeraha yako,/ yakapenya bila huruma Roho yako Takatifu./ Yakaingia kikatili katika Moyo wako Mtakatifu/ hata ukakatika,/ ukapumua Roho yako,/ ukainama Kichwa,/ ukaweka Roho yako mikononi mwa Mungu, Baba yako./ Na baada ya kufa uliacha nyuma Mwili baridi./

Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa Damu yako azizi na kwa kifo chako kitakatifu/ ulizifidia roho za watu,/ ukazitoa ugenini/ na kuzipeleka kwa hisani yako katika uzima wa milele./

Milele uheshimiwe, Wewe Bwana wangu Yesu Kristo./ Siku ya tatu ulifufuka katika wafu,/ ukajionyesha kwa wafuasi wako,/ ukapaa mbinguni/ mbele ya macho yao siku ya arobaini./

Shangilio na sifa ya milele upate Wewe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa umewapelekea wafuasi wako mioyoni mwao/ Roho Mtakatifu,/ ukawasha rohoni mwao mapendo makuu ya Mungu./

Pia, utukuzwe, usifiwe na kushangiliwa milele, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umekaa katika ufalme wako wa mbinguni/ juu ya kiti cha enzi cha Umungu wako,/ ukaishi pamoja na Viungo vyako vyote Vitakatifu./ Na hivyo utakuja tena/ kuzihukumu roho za wazima na wafu wote./ Unaishi na kutawala/ pamoja na Baba na Roho Mtakatifu,/ milele. Amina.

(Na Mt. Birgita wa Sweden)

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Feb 26, 2019
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest May 29, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Mar 11, 2018
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Jan 14, 2018
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Nov 29, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Nov 12, 2017
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Sep 26, 2017
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Sep 2, 2017
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Jul 14, 2017
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ George Mallya Guest Jul 6, 2017
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Jun 22, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Mar 15, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Feb 4, 2017
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Nov 5, 2016
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Nov 5, 2016
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Nov 1, 2016
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Oct 15, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest May 10, 2016
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Mar 19, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Feb 25, 2016
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Feb 13, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Jan 16, 2016
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Jan 14, 2016
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About