Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.
Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.
Sali ‘Salamu Malkia’ na kuongezea, ‘Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.
P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.
Lucy Kimotho (Guest) on September 20, 2017
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
Tabitha Okumu (Guest) on August 24, 2017
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Isaac Kiptoo (Guest) on August 13, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Miriam Mchome (Guest) on July 16, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rose Kiwanga (Guest) on June 30, 2017
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
James Mduma (Guest) on June 3, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rose Kiwanga (Guest) on May 29, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Christopher Oloo (Guest) on April 30, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Anna Malela (Guest) on December 5, 2016
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Lydia Mahiga (Guest) on November 14, 2016
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
Frank Macha (Guest) on September 8, 2016
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Sarah Karani (Guest) on August 11, 2016
Rehema hushinda hukumu
Charles Mchome (Guest) on August 11, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Joyce Aoko (Guest) on July 11, 2016
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Diana Mallya (Guest) on April 11, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Joseph Mallya (Guest) on December 4, 2015
🙏🙏🙏
Hellen Nduta (Guest) on November 5, 2015
Nakuombea 🙏
Peter Mbise (Guest) on October 23, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Peter Mbise (Guest) on September 23, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Esther Cheruiyot (Guest) on August 25, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Francis Mrope (Guest) on May 23, 2015
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nancy Kawawa (Guest) on May 7, 2015
Dumu katika Bwana.
Esther Nyambura (Guest) on April 3, 2015
🙏🌟 Mbarikiwe sana