Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.

Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.

Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.

Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.

Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

Baba yetu… …..Salamu Maria….…Atukuzwe Baba………

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Jul 14, 2024
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Apr 30, 2024
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Mar 13, 2024
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Jan 14, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Oct 20, 2023
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Sep 17, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Sep 14, 2023
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest Aug 31, 2023
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Jul 1, 2023
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jun 19, 2023
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest May 25, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Apr 24, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Mar 21, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Mar 12, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Nov 27, 2022
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Nov 2, 2022
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ Francis Mtangi Guest Oct 6, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ George Mallya Guest May 12, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Apr 17, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Mar 15, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Stephen Mushi Guest Feb 1, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Dec 22, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Dec 10, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Nov 7, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Nov 6, 2021
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Aug 27, 2021
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Jun 23, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ John Lissu Guest Apr 13, 2021
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Feb 14, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Feb 9, 2021
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Jan 6, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Dec 8, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ George Tenga Guest Dec 1, 2020
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Nov 11, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Aug 23, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Aug 2, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Jul 18, 2020
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest May 7, 2020
Amina
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Apr 20, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Mar 6, 2020
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Feb 18, 2020
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Aug 24, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Jun 29, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest May 24, 2019
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Apr 30, 2019
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Mar 21, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Mar 10, 2019
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Feb 27, 2019
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Nov 27, 2018
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest Nov 7, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Oct 27, 2018
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Oct 20, 2018
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ Ann Wambui Guest Oct 13, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest May 28, 2018
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Apr 15, 2018
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Jan 13, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Jan 5, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Nov 14, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Nov 6, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Nov 2, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About