Siri ya Yesu: Mwangaza Wa Maisha

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-12-20 06:33:00πŸ’¬ 100 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Siri ni hii, Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza. Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu. Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu. Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Kujikabidhi Kwa Yesu Kristu Yeye Aliye Mwangaza Wa Maisha

Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza

Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu.
Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu.
Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Yesu Kristu ni mwangaza wa maisha yetu, akiwepo giza lote hutoweka.
Yesu akiwepo hakuna haja ya kufukuza giza bali giza litatoweka Lenyewe.

Unapomkaribisha Yesu katika maisha yako umekaribisha mwanga katika maisha yako na utashinda dhambi na uovu kwa kuwa Yesu aliye mwanga atavifutilia mbali.

Kikubwa ni kumkaribisha Yesu katika maisha yako na kumruhusu atawale Maisha yako na kila kitu katika maisha yako. Ukiweza kuachilia yote kwa Bwana Yesu na kumpa maisha yako basi utashinda uovu/dhambi. Vile unavyojiweka karibu na Yesu ndivyo unavyoshinda dhambi na uovu wote.

Kumkabidhi Yesu MaishaΒ ni Kuamua kuishi kulingana na Mafundisho yake, kuachilia yote katika maongozi yake, kumshirikisha Yesu kwenye kila kitu katika maisha yako na Kuwa mkweli na muwazi mbele ya Yesu katika kila kitu.

Unapomkabidhi Yesu Maisha yako na vyote ulivyonavyo yeye huyatakatifuza na kuyafanya yawe kama yanavyotakiwa kuwa kitakatifu.

Changamoto kubwa kwa Wakristu ni kushindwa kujiweka Mikononi mwa Yesu kwa kuachilia yote na kukabidhi yote kwake. Wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ubinafsi na uchu wa kusimama wenyewe. Wengine wanashindwa kwa sababu ya kukosa Imani. Hawana uhakika kwamba wanachokifanya wanakifanya kweli.

Lakini ukiweza kweli kumkabidhi Yesu Maisha yako, kila kitu kinakua sawa na utafanikiwa kwenye kila kitu. Utaanza kuona unashinda uovu na dhambi kulingana na vile unavyojikabidhi na kujiachilia kwa Yesu.

Anza leo kujikabidhi kwa yesu kwa kiasi kile unachoweza. Yesu anaelewa ubinadamu na madhaifu yetu. Atakusaidia. Hata kama kuna wakati unaweza kujikabidhi kwake na kisha unaanguka tena, yeye ni mwenye huruma na ni mwelewa haswa kuhusu hali yako, atakusaidia na kukuwezesha. Weka nia ya kujikabidhi kwake na kisha utaendelea kidogo kidogo mpaka utajikuta umejikabidhi mikononi kwake kabisa.

KUMBUKA:Β Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza, mwanga ukiwepo giza halibaki linaondoka. Hata siku moja Giza haliwezi kuuzidi mwanga

Uwe na Imani basi, Mtumainie Yesu Kristu atakushindia uovu.

Yesu ndiyo dawa ya uovu na dhambi, kila unapoanguka dhambini mkimbilie yeye naye atakusamehe na kukuwezesha kushinda dhambi na uovu. Usichoke, kila siku jaribu na kujaribu mpaka utashinda.

Nami nakuombea kwa Jina Takatifu la Yesu, Akushindie Uovu na dhambi

πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

100 comment(s)
N
Nicholas Wanjohi2017-02-21 05:03:22
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
J
Jane Muthoni2016-12-31 08:30:59
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
P
Patrick Akech2016-12-30 11:05:02
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
A
Alex Nyamweya2016-12-13 04:44:27
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
E
Elizabeth Mrema2016-12-01 12:34:45
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
H
Henry Mollel2016-11-27 20:58:29
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
I
Irene Akoth2016-10-18 17:21:57
Rehema zake hudumu milele
S
Samuel Were2016-07-29 09:55:06
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
L
Lydia Mahiga2016-03-22 22:48:42
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
L
Lucy Mushi2016-03-05 12:40:32
Tembea kwa imani, si kwa kuona
G
Grace Minja2016-01-23 03:22:00
Baraka kwako na familia yako.
E
Elizabeth Mtei2016-01-21 19:30:39
Neema na amani iwe nawe.
R
Robert Okello2015-10-26 11:28:27
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
S
Sharon Kibiru2015-08-25 12:46:16
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
L
Lydia Mzindakaya2015-08-12 07:53:20
Mwamini katika mpango wake.
R
Rose Mwinuka2015-07-11 02:42:01
Baraka kwako na familia yako.
N
Nancy Kabura2015-07-07 21:48:25
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
G
Grace Majaliwa2015-05-10 05:28:55
Imani inaweza kusogeza milima
M
Mary Njeri2015-05-08 05:10:22
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
R
Richard Mulwa2015-04-30 16:44:40
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi