Siri ya Yesu: Mwangaza Wa Maisha

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-12-20 06:33:00πŸ’¬ 100 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Siri ni hii, Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza. Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu. Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu. Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Kujikabidhi Kwa Yesu Kristu Yeye Aliye Mwangaza Wa Maisha

Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza

Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu.
Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu.
Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Yesu Kristu ni mwangaza wa maisha yetu, akiwepo giza lote hutoweka.
Yesu akiwepo hakuna haja ya kufukuza giza bali giza litatoweka Lenyewe.

Unapomkaribisha Yesu katika maisha yako umekaribisha mwanga katika maisha yako na utashinda dhambi na uovu kwa kuwa Yesu aliye mwanga atavifutilia mbali.

Kikubwa ni kumkaribisha Yesu katika maisha yako na kumruhusu atawale Maisha yako na kila kitu katika maisha yako. Ukiweza kuachilia yote kwa Bwana Yesu na kumpa maisha yako basi utashinda uovu/dhambi. Vile unavyojiweka karibu na Yesu ndivyo unavyoshinda dhambi na uovu wote.

Kumkabidhi Yesu MaishaΒ ni Kuamua kuishi kulingana na Mafundisho yake, kuachilia yote katika maongozi yake, kumshirikisha Yesu kwenye kila kitu katika maisha yako na Kuwa mkweli na muwazi mbele ya Yesu katika kila kitu.

Unapomkabidhi Yesu Maisha yako na vyote ulivyonavyo yeye huyatakatifuza na kuyafanya yawe kama yanavyotakiwa kuwa kitakatifu.

Changamoto kubwa kwa Wakristu ni kushindwa kujiweka Mikononi mwa Yesu kwa kuachilia yote na kukabidhi yote kwake. Wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ubinafsi na uchu wa kusimama wenyewe. Wengine wanashindwa kwa sababu ya kukosa Imani. Hawana uhakika kwamba wanachokifanya wanakifanya kweli.

Lakini ukiweza kweli kumkabidhi Yesu Maisha yako, kila kitu kinakua sawa na utafanikiwa kwenye kila kitu. Utaanza kuona unashinda uovu na dhambi kulingana na vile unavyojikabidhi na kujiachilia kwa Yesu.

Anza leo kujikabidhi kwa yesu kwa kiasi kile unachoweza. Yesu anaelewa ubinadamu na madhaifu yetu. Atakusaidia. Hata kama kuna wakati unaweza kujikabidhi kwake na kisha unaanguka tena, yeye ni mwenye huruma na ni mwelewa haswa kuhusu hali yako, atakusaidia na kukuwezesha. Weka nia ya kujikabidhi kwake na kisha utaendelea kidogo kidogo mpaka utajikuta umejikabidhi mikononi kwake kabisa.

KUMBUKA:Β Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza, mwanga ukiwepo giza halibaki linaondoka. Hata siku moja Giza haliwezi kuuzidi mwanga

Uwe na Imani basi, Mtumainie Yesu Kristu atakushindia uovu.

Yesu ndiyo dawa ya uovu na dhambi, kila unapoanguka dhambini mkimbilie yeye naye atakusamehe na kukuwezesha kushinda dhambi na uovu. Usichoke, kila siku jaribu na kujaribu mpaka utashinda.

Nami nakuombea kwa Jina Takatifu la Yesu, Akushindie Uovu na dhambi

πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

100 comment(s)
C
Charles Wafula2018-06-06 04:01:58
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
L
Lydia Mutheu2018-06-05 08:57:03
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
R
Richard Mulwa2018-06-01 18:48:31
Tumaini ni nanga ya roho
R
Ruth Kibona2018-05-24 12:26:03
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
A
Alex Nakitare2018-04-21 07:09:17
Dumu katika Bwana.
G
Grace Mligo2018-04-04 10:07:13
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
N
Nora Lowassa2018-03-12 03:12:52
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
B
Betty Cheruiyot2018-02-19 08:22:17
Nguvu hutoka kwa Bwana
G
Grace Wairimu2018-02-11 14:07:01
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
P
Patrick Akech2018-02-09 14:56:51
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
M
Mariam Kawawa2017-12-14 10:06:52
Endelea kuwa na imani!
E
Elizabeth Mrope2017-12-07 18:27:53
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
N
Nancy Kawawa2017-12-01 21:21:34
Mwamini katika mpango wake.
R
Ruth Kibona2017-09-22 08:54:24
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
S
Stephen Malecela2017-09-22 06:31:19
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
D
Diana Mumbua2017-09-10 03:20:44
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
J
John Mwangi2017-07-23 07:05:41
Neema ya Mungu inatosha kwako
S
Susan Wangari2017-06-10 21:44:52
Kwa Mungu, yote yanawezekana
G
Grace Minja2017-04-15 00:20:26
Nakuombea πŸ™
J
Jane Malecela2017-03-02 04:50:49
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia