Amri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-12-19 12:25:00πŸ’¬ 51 comments⏱️ ~3 min read
πŸ“„ PDF

Amri kumi za Mungu ni zipi?

1. Ndimi Bwana, Mungu wako usiabudu miungu wengine.
2. Usiape bure kwa jina la Mungu wako.
3. Fanya siku ya Mungu

4. Waheshimu Baba na Mama, upate miaka mingi na heri duniani.
5. Usiue
6. Usizini
7. Usiibe
8. Usiseme uongo
9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10. Usitamani mali ya watu.


Je, ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu?

Ndiyo. Ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu hata kama si Mkristo kwa sababu Mungu ni mkubwa wa watu wote. (Kut 20:1-17, Kumb 5:1-21)


Kwa nini Mungu alitupa Amri kumi?

Mungu alitupa amri kumi ili kutufudisha mambo yatupasayo kwa Mungu, kwa watu na kwetu sisi wenyewe


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusadiki kuwa Mungu ni mmoja, ndiye Baba yetu na Mkubwa wetu: tumpende, tumwabudu yeye peke yake. (Mt 10:33, Kumb 6:4-9)


Wakatoliki tunamwabudu Mungu kwa namna gani?

Tunamwabudu Mungu kwa sala , sadaka na matendo mema


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumekatazwa nini?

Tumekatazwa kumdharau Mungu na kuweka imani yetu katika viumbe badala ya Mungu.


Je, kuna viumbe ambavyo tunaviheshimu kwa kumtukuza Mungu?

Ndiyo twamuheshimu Bikira Maria, Malaika na Watakatifu.


Kwa nini yatupasa kuwaheshimu Watakatifu?

Kwa sababu hao ni washindi, rafiki wa Mungu na waombezi wetu.


Je, tuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu?

Hatuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu tunawaheshimu tu.


Je sanamu zimekatazwa?

Sanamu hazijakatazwa, ila tunaziheshimu kwa sababu zinatukumbusha Mungu na Watakatifu. (Kut 25:18-22).

18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. 19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku. 20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. 21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. Kutoka 25 :18-22.

Vile vile Mungu alishawahi kuwaagiza Waisraeli Wachonge sanamu ya nyoka na yeyote atakayeumwa na nyoka akiiangalia atapona.


Mfano wa sanamu takatifu ni zipi?

Sanamu ya Bikira Maria, Mtoto Yesu, Mt. Yosefu, Moyo wa Yesu na za Watakatifu.


Ni nanai ana kosa kumuabudu Mungu?

Anayekosa kumuabudu Mungu ni yule;

1. Anayeacha kusali au anayesali hovyo
2. Anayemkufuru Mungu
3. Anayeamini na kushika mambo ya kipagani


Mambo gani yanavunja amri ya kwanza ya Mungu?

Mambo hayo ni;

1. Kuabudu sanamu
2. Kufanya matambiko
3. Kwenda kwa waganga
4. Kupiga bao au ramli
5. Kuvaa hirizi
6. Kushiriki mambo ya kichawi n.k.


Ni nini maana ya kuabudu sanamu?

Kuabudu sanamu ni kukipa kiumbe chochote heshima au upendo anaostahili Mungu peke yake.

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

51 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
B
Bernard Oduor2021-04-14 05:38:20
Mungu akubariki!
J
Jacob Kiplangat2021-01-06 17:55:18
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
R
Rose Mwinuka2020-10-28 05:26:02
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
N
Nancy Akumu2020-09-27 15:47:44
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
J
John Kamande2020-09-15 15:20:52
Kwa Mungu, yote yanawezekana
G
Guest2025-12-21 11:40:39
15
N
Nora Kidata2020-07-18 13:54:01
Rehema zake hudumu milele
B
Betty Cheruiyot2020-07-06 04:54:35
Imani inaweza kusogeza milima
M
Mary Kidata2020-06-29 15:27:48
Mwamini Bwana; anajua njia
P
Patrick Akech2020-04-22 12:52:22
Sifa kwa Bwana!
G
George Ndungu2020-02-22 03:36:34
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
T
Thomas Mwakalindile2019-10-09 11:42:33
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
V
Victor Kamau2019-08-10 22:46:50
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
F
Fredrick Mutiso2019-06-29 19:20:02
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
F
Francis Njeru2019-05-29 23:52:47
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
S
Samuel Omondi2019-05-10 01:54:52
Rehema hushinda hukumu
D
Dorothy Mwakalindile2019-02-04 13:39:12
Dumu katika Bwana.
N
Nora Lowassa2018-03-17 21:10:03
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
F
Frank Sokoine2017-11-26 12:13:55
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
A
Alice Wanjiru2017-11-19 18:41:30
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
S
Susan Wangari2017-10-24 15:21:39
Mungu ni mwema, wakati wote!