Log in to access your menu with tools for managing ๐ tasks, ๐ฅ clients, ๐ฐ finances, ๐ learning, ๐ personal growth, and ๐ spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Bakari ni house boy mara nyingi huiba wine ya boss wake na kisha kuongeza maji kwenye chupa ili boss asigundue. Mara kadhaa boss alihisi ladha tofauti anapokunywa wine hivyo kuhisi kuna mchezo mchafu alihisi tu Bakari anahusika. Ilikua ni bahati tu alimvizia na kumbamba Bakari akichakachua wine, kwa kuwa mkewe alikua
Updated at: 2024-05-25 18:06:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Bakari ni house boy mara nyingi huiba wine ya boss wake na kisha kuongeza maji kwenye chupa ili boss asigundue. Mara kadhaa boss alihisi ladha tofauti anapokunywa wine hivyo kuhisi kuna mchezo mchafu alihisi tu Bakari anahusika. Ilikua ni bahati tu alimvizia na kumbamba Bakari akichakachua wine, kwa kuwa mkewe alikua anamtetea Bakari, ili kumthibitishia mkewe kuwa Bakari ndo culprit, boss alianza kwa kumuuliza Bakari maswali. Siku hiyo Bakari alikua jikoni, boss na mkewe walikua sebuleni.
Boss akaamua amfuate hukohuko jikoni. Boss: Kwanini nikikuita unaitikia, nikikuuliza unanyamaza? Bakari: baba huku jikoni ndo kulivyo, unasikia jina tu likiitwa lakini maneno menginehusikii, na kama huamini baki jikoni mi niende sebuleni.
Bakari akaenda sebuleni akaanza kuita. Bakari:Babaa! Boss: naam Bakari! Bakari: Saa sita usiku huwa unaenda kufanya nini chumba cha house girl?
Boss kimyaaaa! Bakari: Baba babaa! Boss:ndio Bakari! Bakari: Nauliza hivii, chumbani kwa house girl saa sita za usiku huwa wafuata nini?
Boss kimyaaaaaaa! Boss akatoka nje: Bakari huku jikoni ni kweli husikii kitu zaidi ya jina!
Mke wa Boss akaingilia kati Mama: nyie msinitanie kabisa mnasemaje? Bakari: kweli mama ukiwa jikoni husikii kitu nenda uone
Mama akaenda na Bakari akaanza
Bakari: mamaaaa! Mama: abeee! Bakari: hebu niambie hiyo mimba ni ya baba au yangu? Mama kimya
Bakari: mamaaaa! Mama: abeeee! Bakari: hebu niambie ukweli hiyo mimba ni ya baba au yangu?? Mama kimya
Mama akatoka nje: kweli humu jikoni kuna tatizo nilikuwa nasikia jina tu
Hii ndio ndoto ya harusi ya kila msichana anayotamani
GIRL: Baby, hebu niambie harusi yetu itakuwaje?
BOY: Yaani hii haijawahi kushuhudiwa, ngoja nikupe kionjo kidogo tu
GIRL: Enheeโฆ
BOY: Kwanza siku ya kupeleka mahari nitaswaga zizi zima la ng'ombe napeleka kwa babu yako
GIRL: Ooh baby u care..
Updated at: 2024-05-25 18:05:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
GIRL: Baby, hebu niambie harusi yetu itakuwaje?
BOY: Yaani hii haijawahi kushuhudiwa, ngoja nikupe kionjo kidogo tu
GIRL: Enheeโฆ
BOY: Kwanza siku ya kupeleka mahari nitaswaga zizi zima la ng'ombe napeleka kwa babu yako
GIRL: Ooh baby u care..
BOY: Siyo hivyo tu, baba yako ntamnunulia Range Rover Sport na mama mkwe ntampa Range Rover Evoque
GIRL: Baby u are awesomeโฆ
BOY: Halagu mdogo wako wa kiume ntampa Prado Tx, na hapo nimesukutua tu mdomo sijaanza kulaโฆ.
GIRL: Enheeโฆna sisi??
BOY: Sisi tutachukua mtaa mzima Oysterbay, kila wiki tutaishi nyumba tofauti
Halafu siku ya harusi yetu tutakodi zile meli zinabeba makontena ndiyo iwe ukumbi wetu, itatupeleka hadi Maldives
GIRL: Baby I love you
BOY: Tukitoka hapo tunaenda honeymoon Bahamasโฆ.halafu tunaenda Taiwan shopping ya fenicha, kisha Japan shopping ua electronics, halafu tunaenda Dubai nikununulie vito vya thamani
GIRL: Ooh my sweetheartโฆhalafu tukitoka huko??
BOY: Tukitoka huko nachukua ndoo ya maji nakumwagia uzinduke usingizini na ndoto yako imeishia hapo
Nilichokifanya jana baada ya kushuka kwenye basi Ubungo
Updated at: 2024-05-25 17:02:05 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jana nateremka kwenye BASI UBUNGO nataka nichukue TEKSI hadi KIMARA naambiwa sh.15,000/=. Wakati niponatafakari hiyo bei, nikasikia "Moro, Moro,Morogoro sh.6,000/="
Nikaamua nipande niende zangu MOROGORO. Kwenda na kurudi sh.12,000/=. Wakati wa kurudi nikamwmbia KONDA aniteremshe KIMARA.
Angalia alichojibu huyu mwanafunzi, Ungekua wewe ni mwalimu wake ungemfanyaje?
Updated at: 2024-05-25 17:55:55 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mwanafunz alikuwa kila siku anachelewa shule, na kila siku alikuwa anachapwa, basi siku moja mwalimu akaona ngoja amuulize.
Mwalimu: Mbona unachelewa kila siku? Mwanafunzi: Nakaa mbali mwalimu Mwalimu: (huku ana hasira akauliza)Mbali mbinguni? Mwanafunzi: Mbinguni kwa mbele๐๐๐๐๐
Updated at: 2024-05-25 17:48:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Tukiwa kanisani mdada alikuwa amelala , akaamka akasikia Pastor anasema " SIMAMA" Yule dada akasimama akashangaaa kanisa zima linamtizima kwa mshangao akiwemo mumewe, akaangalia kanisa zima akashtuka kujiona yeye peke yake ndiye aliesimama Pastor akaendelea vizur endelea kusimama, tumepata mmoja hadi sasa aliyesimama narudia kwa mara ya mwisho kama hujasikia vizuri " kama wew umewahi kumsaliti au bado unasaliti ndoa yako SIMAMA" Binti akazimia
Huyu mke kwa kupenda hela! Cheki anachomwambia mume wake
Jamaa karudi toka kazini mpole na hana furaha!
MKE; Vipi leo mbona mpole?
MUME; Ofisi yetu imeungua na watu wote waliokuwemo wamekufa.
MKE; Ilikuaje wewe ukapona?
Updated at: 2024-05-25 18:02:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Jamaa karudi toka kazini mpole na hana furaha!
MKE; Vipi leo mbona mpole?
MUME; Ofisi yetu imeungua na watu wote waliokuwemo wamekufa.
MKE; Ilikuaje wewe ukapona?
MUME; Nilikua chooni jirani na ofisi najisaidia.
MKE; Loh maskini, familia zao itakuaje?
MUME; Watalipwa million 100 kila mfiwa.
MKE; KWA HASIRA, Ona sasa na wewe kunya kunya kwako umetukosesha mihela.. Ungeenda kunya akhera.
Updated at: 2024-05-25 17:05:08 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Leo nikaamua niingie misa ya asubuhi kwenye kanisa moja la kilokole kulikua na ugeni wa mchungaji kutoka Bulgaria, Mahubiri yameanza saa 1 asubuhi hali ikawa kama hivi:
MCHUNGAJI: My name is Pastor Livingstone MKALIMANi: Kwa jina naitwa mchungaji Jiwe linaloishi MCHUNGAJI: We thank God for All goals we set by our hands MKALIMANI: Tunamshukuru Mungu kwa Magoli yote tuliyoweka kwa Mkono
Hivi navyoongea kanisa halina viti waumini wote tumekimbia nje naona Mkalimani amebaki na kiatu cha kushoto tu. Sunday joke