Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga wa ngano - 2 - 2 ¼ Vikombe
Siagi - 1 ½ Kikombe
Sukari - 1 Kikombe
Yai - 1
Vanilla -Tone moja
Baking Powder -kijiko 1 cha chai
Chumvi - Kiasi kidogo (pinch)
Unga wa Kastadi - 2 Vijiko vya supu
MATAYARISHO
Changanya vitu vyote isipokuwa unga. Tia unga kidogo kidogo mpaka mchanganyiko uwe sawa. Kisha fanya duara ndogo ndogo uzipange kwenye treya na utie rangi katikati. Halafu zichome katika moto wa 300°F kwa muda wa dakika 20 - 25 na zisiwe browni . Kisha panga kwenye sahani tayari kuliwa na chai.
Updated at: 2024-05-25 10:23:00 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) vikombe 2 na1/2 Sukari (sugar) 1/2 kikombe Hamira (yeast) 1/2 kijiko cha chai Hiliki (cardamon powder) 1/4 kijiko cha chai Tui la nazi (coconut milk) kiasi Baking powder 1/4 kijiko cha chai Siagi (butter)1 kijiko cha chakula Mafuta ya kukaagia
Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote kasoro tui la nazi na mafuta ya kukaangia. Ukisha changanyika vizuri tia tui la nazi na uanze kuukanda mpaka uwe mlaini. Baada ya hapo usukume na ukate mandazi katika shape uipendayo, Kisha uyawe katika sehemu yenye joto (warm place) ili yapate kuumuka. Yakisha uumuka yakaange katika mafuta mpaka yaive kisha ipua na uyaache yapoe tayari kwa kuliwa. (Mafuta ya kukaangia yasiwe yamoto sana kwani yatayababua mandazi na hivyo ndani hayataiva vizuri.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Miguu ya kuku (chicken legs) 10 Kitunguu swaum na tangawizi (ginger & garlic paste) 1 kijiko cha chakula Limao (lemon) 1 Pilipili iliyosagwa (ground scotch bonnet) 1/2 Giligilani iliyokatwakatwa (chopped coriander) kiasi Chumvi (salt) kiasi Mafuta ya kukaangia (veg oil)
Matayarisho
Safisha kuku kisha mtie kwenye sufuria na viungo vyote (kasoro mafuta na giligilani) kisha mchemshe mpaka aive na umkaushe supu yote. Baada ya hapo mkaange katika mafuta mpaka awe wa brown kisha mtoe na uweke katika kitchen towel ili kuchuja mafuta. Baada ya hapo weka katika sahani na umwagie giligilani kwa juu. Na hapo kuku wako atakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Pilipili hoho (Red pepper 3) Cougette 1 Kitunguu (onion 1) Uyoga (mashroom 1 kikombe cha chai) Carrot 1 Nyanya (fresh tomato 1) Nyanya ya kopo iliyosagwa (tomato paste 3 vijiko vya chai) Giligilani (fresh coriander) Binzari manjano (Turmaric 1/2 ya kijiko cha chai) Curry powder 1/2 ya kijiko cha chai Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Kata hoho kati na utoe moyo wake kisha ziweke pembeni, Kisha katakata cougette, kitunguu, uyoga, carrot, nyanya katika vipande vidogo vidogo, Weka sufuria jikoni na uanze kupika uyoga kwa muda wa dakika 5, kisha weka curry powder, turmaric na chumvi na kaanga kidogo kisha weka vegetable zilizobakia pamoja na nyanya ya kusaga pamoja na giligilani. Zikaange kwa muda wa dakika 5 kisha zitie kwenye hoho na kisha uzibake kwa muda wa dakika 20 na hapo zitakuwa tayari kuseviwa na wali. Wali: angalia katika recipe zilizopita
Jinsi ya kupika Mboga Za Majani Makavu (Aina Yoyote)
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Mboga za majani makavu ¼ kg Mafuta vijiko vikubwa 3-4 Karanga zilizosagwa kikombe ½ Maziwa au tui la nazi kikombe 1 Kitunguu 1 Nyanya 2 Chumvi (kama kuna ulazima) Maji baridi
Hatua
• Loweka mboga za majani makavu na maji kwa dakika 10-15. • Osha , mboga na katakata nyanya na vitunguu. • Kangaa, pukusua na saga karanga zilainike. • Kanga kitunguu, weka nyanya, koroga zilainike. • Ongeza mboga zilizolowekwa na maji yake kwenye rojo, koroga na funikia mpaka maji yakaukie na ive. Punguza moto. • Koroga karanga zilizosagwa na maji, ongeza kwenye mboga ukikoroga kwa dakika 5. • Onja chumvi, pakua kama kitoweo. Uwezekano Weka nyanya kidogo. Tumia tui la nazi au krimu badala ya maziwa. Weka nyama au dagaa au Mayai badala ya Karanga.
Updated at: 2024-05-25 10:34:54 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga 2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)
Sukari 1/3 Kikombe cha chai Mayai 5
Siagi 4 Vijiko vya chakula
Hamira 1 Kijiko cha chakula
Baking Powder 1 Kijiko cha chai
Vanilla 1 Kijiko cha chai
Hiliki zilizosagwa 1 Kijiko cha chai
Sukari ya laini ya unga
(icing sugar) 1 Magi
Jinsi ya kuandaa na kupika
Unavunja mayai, unatia sukari, hamira, baking powder, vanilla na hiliki ikisha unapiga kwa kutumia mchapo wa kupigia keki. Unapiga mchanganyiko kwa muda wa dakika tano.
Unatia siagi kwenye sufuria na unaiyayusha na kuipasha moto mpaka iwe moto ikisha unaimimina kwenye mchanganyiko na unapiga tena kwa dakika mbili tu.
Unatia unga kwenye sinia au bakuli kubwa ikisha unamimina ule mchanganyiko kwenye unga na unaukanda kutumia mkono, mpaka ulainike.
Ukiona unga mwingi basi ongeza maziwa kidogo mpaka uwe sawa, na ukiona unga mwepesi sana basi unaweza kuongeza unga kidogo pia mpaka ukae sawa mfano wa unga wa maandazi.
Sukuma na ukate madonge kama unavyoyaona hapo juu. Tumia kifuniko cha chupa kwa kukatia kiduara kidogo katikakti ya madonge. Ukimaliza kukata madonge yote, yaweke kidogo yavimbe halafu teleka mafuta na uyachome. Ukitoa kwenye mafuta yachuje moto na kabla ya kupoa yawe moto moto yarovye kwenye icing sugar na uhakikishe yote yameenea sukari juu. Ukimaliza tia kwenye sahani acha zipowe na zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi inayoharibu afya yako mfano uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe kupita kiasi,kutokufanya mazoezi na kutokula matunda na mbogamboga.
Mambo yanayoweza kukusaidia kuishi maisha marefu ni kama yafuatayo
Kuuandaa mwili kwa maisha marefu kwa kufanya mazoezi
Kuwa makini kutambua na kutibu matatizo ya kiafya
Kuepuka mazingira na kufanya kazi kwa namna au kazi zinazoweza kudhuru maisha yako. Mfano kuendesha gari bila kufuata utaratibu, kutokuvaa vifaa vya kujikinga wakati wa kazi
Epuka vitu vyenye sumu vinavyoweza kudhuru afya yako na kukuletea matatizo ya kiafya kama dawa za mimea na mifugo, zitumie kama inavyotakiwa
Usinywe pombe, usivute sigara wala kutumia dawa za kulevya
Updated at: 2024-05-25 10:22:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula) Maziwa fresh (milk 1/2 kikombe) Sukari (sugar 1/4 ya kikombe cha chai) Siagi (butter kijiko 1 cha chakula) Maji (vikombe 4 vya chai) (serving ya watu wawili)
Matayarisho
Chemsha maji ya uji, Kisha koroga unga na maji ya baridi kiasi na uchanganye kwenye maji ya moto yanayochemka. Endelea kukoroga mpaka uchemke ili kuhakikisha uji haupatwi na madonge. Ukishachemka tia, maziwa, sukari na butter. Kisha acha uchemke kwa muda wa dakika 10 na hapo uji utakuwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele 2 vikombe vya chai Choroko kikombe 1 na 1/2 Nazi kopo 1 Swaum 1 kijiko cha chakula Kitunguu 1 kikubwa Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai Chumvi Mafuta
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima, pindi ukianza kupika loweka mchele nusu saa kisha katika sufuria kubwa, kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia swaum na binzari nyembamba kisha tia choroko, mchele, chumvi,nazi na maji mengi kiasi yakuivisha choroko pamoja na mchele. Pika mpaka vitu vyote viive na viwe vilaini kisha upondeponde kiasi.Baada ya mseto wako kuiva utakuwa unaonekana kama uji wa mchele vile. Na Baada ya hapo mseto wako utakuwa tayari kwa kuliwa na mboga yoyote uipendayo.Inapendeza zaidi kuliwa vile tu ukishamalizwa kupikwa