Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:35 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa basmati - 3 vikombe
Kuku - ½
Viazi - 4
Vitunguu - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu
Binzari ya pilau nzima - 1 Kijiko cha chakula
Binzari ya pilau - ½ kijiko cha chai
Pilipili manga nzima - ½ kijiko cha chai
Karafuu nzima - 8
Iliki nzima - 6
Mdalasini nzima - 5 vijiti
Pilipili mbichi iliyosagwa - 2
Chumvi - kiasi
Mafuta ya kupikia - ¼ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele. Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi. Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria. Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi. Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia. Mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza) Ukishakuwa tayari pakua kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.
Jinsi ya kupika Pilau Ya Nyama Ya Ng'ombe Na Nyanya
Updated at: 2024-05-25 10:35:28 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi
Mchele (Basmati) 3 vikombe
Nyama ya ngo’mbe 1 kg
Pilipili boga 1 kubwa
Nyanya 2 kubwa
Vitunguu maji 2 vikubwa
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa 1 kijiko cha supu
Tangawizi 1 kijiko cha chai
Ndimu 1
Mafuta ya kupikia ½ kikombe
Mdalasini ½ kijiko cha chai
Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai
Pilipili manga ½ Kijiko cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
Jinsi ya kuandaa na kupika
Loweka mchele wako katika chombo
Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi
Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi
katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni
Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia
Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto
Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya
Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi
Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke
Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza
Funika na punguza moto na uache uive taratibu
Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi
Mchele wa basmati - 3 vikombe
Kuku - ½
Bilingani - 2 ya kiasi
Viazi - 4
Vitunguu - 2
Kitunguu (thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 2
Chumvi - kiasi
Garama masala (mchanganyiko wa bizari) - 1 kijiko cha chai
Hiliki ya unga - ¼ kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia wali - ¼ kikombe
Mafuta ya kukaangia viazi na bilingani - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele. Kata kuku vipande upendavyo safisha Kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu, na bizari mchanganyiko (garama masala). Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria. Menya na kata viazi kaanga weka kando. Kata kata bilingani slesi nene kaanga, chuja mafuta weka kando. Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi. Tia vipande vya kuku, ukaange kidogo. Tia supu ya kuku, mchele, tia hiliki, ufunike hadi karibu na kuwiva kabisa. Tia viazi na bilingani uchanganye kidogo, kisha tia katika oven imalizike kupikika pilau humo au unaweza kuendelea kufunika juu ya jiko hadi pilau iwive. Pakua katika sahani ikiwa tayari kuliwa kwa saladi ya mtindi.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Maharage yaliyochemshwa kiasi Spinach zilizokatwa kiasi Vitunguu maji 2 Nyanya 1/2 kopo Swaum/Tangawizi 1 kijiko cha chakula Curry powder 1 kijiko cha chai Olive oil Chumvi
Matayarisho
Kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia tangawizi/swaum kisha nyanya. Pika mpaka nyanya ziive kisha tia curry powder na chumvi. Vipike kiasi kisha tia maharage na maji kidogo kisha funika na uache vichemke. Baada ya muda tia spinach vipike pamoja na maharage mpaka ziive kisha ziipue. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Blue band vijiko vikubwa 2 Maziwa vikombe 2 Royco kijiko kikubwa 1-2 Pilipili manga (unga) kijiko cha 1 Chumvi kiasi Maji lita 2-3 Boga kipande ½ Viazi mviringo 2 Vitunguu 2 Karoti 2 Nyanya 2
Hatua
• Menya boga, viazi, karoti, nyanya na kwaruza weka kwenya sufuria kubwa. • Menya, osha na katakata vitunguu kisha ongeza kwenye mboga. • Ongeza maji na chumvi chemshwa mpaka vilainike. • Pekecha ikiwa jikoni na moto kidogo • Ongeza blue band, maziwa royco na pilipili manga ukikoroga kwa dakika 5. • Onja chumvi na pakua kama supu. Uwezekano Tumia siagi badala ya margarine.
Updated at: 2024-05-25 10:23:04 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (nusu kilo) Sukari (Kikombe 1 cha chai) Chumvi (nusu kijiko cha chai) Hamira (kijiko kimoja cha chai) Yai (1) Maziwa ya unga (vijiko 2 vya chakula) Butter (kijiko 1 cha chakula) Hiliki (kijiko1 cha chai) Maji ya uvuguvugu ya kukandia Mafuta ya kuchomea
Matayarisho
Tia unga kwenye bakuli kisha tia sukari, chumvi, yai, maziwa ya unga, butter na hiliki kisha uchanganye pamoja mpaka mchanganyiko wote uchanganyike vizuri. Baada ya hapo tia maji ya uvuguvugu kiasi na uanze kuukanda. Ni vizuri ukaukanda kwa muda wa dakika 15 ili kuhakikisha donge lote la unga limelainika vizuri. Baada ya hapo Tawanyishaa unga uliokwandwa katika madonge 4. Tia unga wa ngano kidogo katika kibao cha kusukumia na uanze kusukuma donge moja katika shape ya chapati na hakikisha haiwi nyembamba sana wala nene sana yani inatakiwa iwe ya wastani.Ukishamaliza kusukuma unatakiwa ukate shape uipendayo na uyatandaze katika kitu kilichopo flat na kiwe kimenyunyuziwa unga wa ngano ili kuyazuia yasigandie. Rudia hiyo process kwa madonge yote yaliyobakia. Baada ya hapo yaweke mandazi katika sehemu iliyokuwa na joto ili yaweze kuumuka (inaweza kuchukua masaa 3 kuumuka). Yakisha umuka unatakiwa uweke mafuta katika karai la kuchomea. Yakisha pata joto la kiasi unatakiwa utumbukize mandazi na unaze kuyachoma mpaka yawe ya brown. Yakisha iva yaipue na uyaweke kwenye kitchen towel iliyakauke mafuta. Yakisha poa yatakuwa tayari kwa kuliwa.
Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi
Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo Vya Wali
Mchele - 3 vikombe
Tambi - 2 vikombe
Mafuta - ¼ kikombe
Chumvi
Vipimo Vya Kuku
Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande - 1 Kilo
Kitunguu maji kilichokatwa katwa - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Paprika - 1 kijiko cha supu
Masala ya kuku (tanduri au yoyote) - 1 kijiko cha supu
Ndimu - 2 vijiko vya supu
Mtindi (yoghurt) au malai (cream) - 1 kikombe
Mafuta - ¼ kikombe
Majani ya kotmiri (coriander) - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:
Osha Mchele, uroweke. Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu. Tia mchele endelea kukaanga kidogo. Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku
Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu. Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi. Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri. Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.
Updated at: 2024-05-25 10:37:46 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi laini (Matoke 6) Viazi mbatata (potato 3) Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2) Kitunguu swaum (garlic 6 cloves) Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo) Vitunguu (onion 1) Pilipili (chilli 1 nzima) Chumvi (salt to your taste) Mafuta (vegetable oil) Limao (lemon 1/2) Curry powder (1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:40 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi ulaya 4 vya wastani Hoho jekundu 1/2 Hoho la njano 1/2 Hoho la kiajani 1/2 Njegere 1 kikombe cha chai Carrot 1 kubwa Broccoli kidogo Cauliflower kidogo Kitunguu 1 Nyanya 1/2 kopo Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chakula Curry power 1 kijiko cha chakula Coriander powder 1 kijiko cha chai Tarmaric 1/2 kijiko cha chai Olive oil Chumvi 1/4 ya limao
Matayarisho
Katika sufuria isiyoshika chini kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia swaum/tangawizi na spice zote kaanga kwa muda mfupi kisha tia nyanya na chumvi. pika mpaka nyanya ziive kisha tia vegetable zote na vimaji kidogo sana na kisha kamulia limao, baada ya hapo punguza moto na kisha funika na zipike mpaka vegetable zote ziive na rojo ibakie kidogo. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:38 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi - 3lb
Nyama - 1lb
Kitunguu - 1
Nyanya - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 kijiko cha chai
Manjano - ½ kijiko cha chai
Curry powder - ½ kijiko chai
Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai
Pilipili ya unga - kiasi upendavyo
Chumvi - kiasi
Kidonge cha supu - 1
Tui la nazi - 1 kopoau zaidi
Mtindi ukipenda - 3 vijiko vya supu
Kotmiri - kiasi ya kupambia
Nazi ya unga - 4 vijiko vya supu
Mafuta - 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande kisha chemsha na chumvi mpaka iive. Menya maganda viazi na ukate slice kubwa weka pembeni Kata kata kitunguu kisha kaanga na mafuta mpaka vibadilike rangi Tia thomu, bizari ya manjano, pilipili ya unga, nyanya kopo Kata kata nyanya nzima vipande vidogo tia na kidonge cha supu. Kisha tia viazi, nyama na tui la nazi finika mpaka viazi viwive lakini visiwe vikavu. Tia mtindi na nazi ya unga kama vijiko 4 vya supu iache motoni kidogo kisha pakua, tupia kotmiri juu na itakuwa tayari kuliwa.