ACKYSHINE ARTICLE

Maswali na Majibu kuhusu Mafumbo ndani ya Kanisa Katoliki

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… February 16, 2020πŸ’¬ 50 comments
Neno hili kuwa nafsi tatu kwa Mungu mmoja laitwaje?

Laitwa fumbo la Utatu Mtakatifu. (Lk, 3:21-22)


Kanisa linafafanuaje fumbo la umwilisho?

Linatamka kuwa Yesu Kristo ni Mungu kweli na Mtu kweli. (Ebr 4:15)


Nini maana ya neno "Fumbo"?

Fumbo ni ukweli ambao hatuwezi kuelewa kikamilifu, lakini tunasadiki kwa kuwa Mungu hutufumbulia. (Math 11:27)


Katika dini yetu yapo mafumbo hasa mangapi?

Mafumbo matatu

1. Fumbo la Utatu Mtakatifu 2. Fumbo la Mungu Kujifanya mtu 3. Fumbo la Ukombazi wetu