Je, kuna madhara gani kama mtu anakaa muda mrefu bila kujamiiana au kufanya mapenzi?
ποΈ Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salamaπ Kiswahili

Ukweli ni kwamba hakuna madhara yoyote ya kiafya iwapo utakaa muda mrefu bila ya kujamiiana. Viungo vya uzazi havidhuriki wala sehemu nyingine yoyote katika mwili wako. Mwanamke na mwanaume wakianza kujamiiana baada ya kukaa muda mrefu watapata raha na starehe kama kawaida.
Kuna uvumi potofu kwamba kutofanya mapenzi kunasababisha kuwa na chunusi usoni au sehemu za siri, au hata kuchanganyikiwa kiakili. Siyo kweli kwamba hali hiyo inasababishwa na kutojamiiana bali husababishwa na mambo mengine kabisa.
Elewa kwamba kutojamiiana kabisa hakuna madhara yoyote. Lakini kama tulivyosema awali kujamiiana kunaweza kuleta matatizo mengi kama mimba isiyotarajiwa, magonjwa ya zinaa ikiwa pamoja maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe.
β
Direct PDF download
The download button now generates the PDF on the server. It no longer depends on an off-screen browser canvas, so the former blank-PDF capture path is bypassed.