Jinsi ya kupika Pilau Ya Nyama Ya Ng'ombe Na Nyanya
ποΈ Dondoo za Mapishi na LisheποΈ Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya#Karibu AckySHINEπ Kiswahili

Viambaupishi
Mchele (Basmati) 3 vikombe Nyama ya ngoβmbe 1Β kg Pilipili boga 1 kubwa Nyanya 2 kubwa Vitunguu maji 2 vikubwa Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa 1 kijiko cha supu Tangawizi 1 kijiko cha chai Ndimu 1 Mafuta ya kupikia Β½ kikombe Mdalasini Β½ kijiko cha chai Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai Pilipili manga Β½ Kijiko cha chai Hiliki Β½ Kijiko cha chaiJinsi ya kuandaa na kupika
Loweka mchele wako katika chombo Chukuwa nyama na ioshe vizuri na itie thomu, tangawizi, ndimu, pilipili manga na chumvi kiasi Iweke jikoni hadi ikauke maji na kuwa imewiva huku ukiikaanga kaanga kwa hayo hayo mafuta yake hadi kuwa rangi ya hudhurungi katakata Vitunguu na nyanya weka pembeni Chukua pilipili boga, thomu, tangawizi na visage katika mashine ya kusagia Weka sufuria pembeni na utie mafuta, subiri yapate moto Kisha tia vitunguu na vikaange hadi kuwa hudhurungi na tia nyanya Kisha mimina mchanganyiko wako ulio usaga wa pilipili boga, thomu na tangawizi Koroga kwa dakika kadhaa Kisha mininia nyama uliyokuwa tayari, maji kiasi na chumvi wastani na subiri maji hayo yachemke Weka mchele humo na koroga kiasi na onja chumvi kama ipo sawa au kama ndogo unaweza kuongeza Funika na punguza moto na uache uive taratibu Baada ya kukauka maji kabisa basi ugeuze na subiri tena kwa dakika kama mbili na tayari kuliwa.β
Direct PDF download
The download button now generates the PDF on the server. It no longer depends on an off-screen browser canvas, so the former blank-PDF capture path is bypassed.