πMaswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki
Ishara ndogo ya Msalaba juu ya panda la uso, mdomo, na kifua kabla ya Injili ina maana gani?
Maana yake ni kama Ahadi kuwa, Niko tayari kulifahamu Neno la Mungu kwa akili yangu, Nitalitangaza kishujaa kwa Midomo yangu, Nitalipenda na kulishika kwa Moyo wangu wote.
Open printable article βπMaswali na majibu kuhusu Katekesi
Katekista ni nani?
Katekista ni mlei aliyechaguliwa na Kanisa ili kumfanya Kristo ajulikane, apendwe, na kufuatwa na wale ambao hawajamfahamu na pia waamini
Waraka wa Baba Mtakatifu Unatafsiri vipi Makatekista?
Waraka unasema;
1. Makatekista ni Wafanyakazi maalimu
2. Mashahidi wa moja kwa moja, Wainjilishaji wasio na mbadala
Open printable article βπMaswali na Majibu kuhusu Rehema
Rehema ni nini?
Rehema ni msamaha au ondoleo la adhabu ya dhambi tulizostahili sababu ya dhambi zilizokwisha ondolewa
Open printable article βπMafundisho kuhusu Toharani
Toharani ni mahali gani?
Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi.
Open printable article βπAmri ya Kumi ya Mungu: Makatazo na Amri
Amri ya Kumi ya Mungu inaamuru kuheshimu mali ya wengine na kumpenda Mungu kupita vitu vyote
Open printable article βπAmri ya Nane ya Mungu: Makatazo na Amri
Katika Amri ya Nane Mungu anaamuru tuseme ukweli na tulinde heshima ya wengine. (Mt 5:37, Yak 5:12).
Open printable article βπAmri ya Tano ya Mungu: Kutunza uhai wetu na wa watu wengine
Katika Amri ya Tano ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa tutunze uhai wetu na wa watu wengine tangu mwanzo hadi mwisho. (Mwa 4:10-11)
Kwa nini ni lazima kutunza uhai wetu na wa wenzetu?
Kwa sababu uhai wa watu wote umetoka kwa Mungu
Open printable article βπAmri ya nne ya Mungu: Kuheshimu Wazazi
Katika Amri ya nne ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa tuwaheshimu wazazi wetu na wakubwa wetu wote, tuwapende, tuwatii na tuwaombee. (Kut 20:12, Kol 3:20)
Amri ya Nne ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa tuwaheshimu wazazi wetu na wakubwa wote, tuwapende, tuwatii na tuwaombee. (Kut 20:12), Kol 3:20
Open printable article βπAmri ya Pili ya Mungu: Tunakatazwa kuapa bure au uongo kwa Jina la Mungu
Katika amri ya pili ya Mungu tumekatazwa nini?
Katika amri ya pili ya Mungu tunakatazwa kuapa bure kwa Jina la Mungu
Kiapo cha uongo ni nini?
Ni kuahidi kwa kiapo bila nia ya kutimiza au kuvunja ahadi iliyotelewa.
Open printable article βπAmri za Kanisa: Mambo ya Muhimu kujua na Kuzingatia
Amri za kanisa ni;
1. Hudhuria Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka
5. Saidia Kanisa Katoliki kwa zaka
6. Shika sheria Katoliki za ndoa.
Open printable article βπMambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Ishara ya Msalaba
Ishara ya msalaba ni nini?
Ishara ya Msalaba ni tendo la mtu kugusa panda la uso, kifua na mabega kwa kutumia mkono wa kulia na kutamka βKwa jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Aminaβ
Open printable article βπMafundisho kuhusu Neema
Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)
Open printable article βπAmri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu
Haya ni Mafundisho Muhimu kuhusu Amri kumi za Mungu unayopaswa kufahamu.
Open printable article βπAmri ya Kwanza ya Mungu: Mambo Muhimu ya Kuzingatia
Katika amri ya kwanza ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa tusadiki kuwa Mungu ni mmoja, ndiye Baba yetu na Mkubwa wetu: tumpende, tumwabudu yeye peke yake. (Mt 10:33, Kumb 6:4-9)
Wakatoliki tunamwabudu Mungu kwa namna gani?
Tunamwabudu Mungu kwa sala , sadaka na matendo mema
Open printable article βπAmri ya Tatu ya Mungu: Tumeamriwa kuheshimu siku ya Mungu
Katika amri ya tatu ya Mungu tumeamriwa nini?
Tumeamriwa kuheshimu siku ya Mungu:-
1. Kushiriki Misa Takatifu siku ya Jumapili na Sikukuu zote za Amri
2. Kuacha kazi nzito na
3. Kutenda matendo mema
Open printable article β