Mafundisho kuhusu Neema

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-02-28 03:33:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF
Je, tunaweza kuhakikisha neema ya utakaso?
Hapana, hatuwezi kuhakikisha neema ya utakaso kwa kuwa ni tukio ambalo linapita maumbile na kufanyika rohoni, hivyo halifikiwi na hisi zetu. Pengine Mungu anatokeza dalili fulani za badiliko hilo kama vile furaha ya ndani au karama ya nje, lakini hizo hazihitajiki wala hazitoshi kuthibitishia mtu amepata neema hiyo.
β€œWengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu” (Math 7:22-23).
β€œNijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu” (1Kor 13:1-3).

Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)

Kuna aina ngapi za neema?
Kuna aina mbili za neema
1. Neema ya utakaso 2. Neema ya msaada

Neema ya Utakaso ni nini?
Neema ya Utakaso ni uzima wa Kimungu unaomiminwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu. (Yoh 1:16, Yoh 3:3-5)

Neema ya Utakaso yapatikanaje?
Neema ya Utakaso yapatikana kwa; 1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo 2. Sakramenti ya Kitubio 3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
4. Yaongezwa kwa kupokea Sakramenti nyingine 5. Kwa Sala 6. Kwa Ibada Takatifu 7. Kwa matendo mema

Neema ya Utakaso yapoteaje?
Neema ya Utakaso yapotea kwa kutenda dhambi kubwa (dhambi ya mauti)

Kuna Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso?
Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso ni;-
1. Kupendwa na Mungu hapa duniani 2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa

Neema ya Msaada ni nini?
Neema ya Msaada ni msaada tupatao kwa Roho Mtakatifu kutuongezea nguvu Rohoni tutende mambo mema na tuepuke Mabaya

Neema ya Msaada yapatikanaje?
Neema ya Msaada yapatikana kwa kupokea Sakramenti, kusali, na kutenda mambo ya Ibada (Yoh 15:5, 1Tim 2:4)
πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

50 comment(s)
J
John Lissu2024-07-22 14:51:45
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
J
Janet Sumari2024-04-18 01:43:08
Kwa Mungu, yote yanawezekana
B
Betty Cheruiyot2024-04-07 22:03:37
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
S
Stephen Kikwete2024-04-06 23:58:56
Mwamini katika mpango wake.
V
Vincent Mwangangi2024-01-28 09:37:54
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
J
Joy Wacera2024-01-11 11:56:12
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
K
Kenneth Murithi2023-11-30 14:12:43
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
A
Alice Jebet2023-11-13 04:48:28
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
R
Ruth Mtangi2023-09-11 04:56:09
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
S
Samuel Omondi2023-05-26 22:28:12
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
S
Sarah Karani2023-05-04 08:39:22
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
F
Frank Sokoine2023-02-27 21:33:37
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
E
Edward Lowassa2023-01-13 13:20:44
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
S
Stephen Mushi2023-01-09 17:16:08
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
S
Stephen Malecela2022-10-04 15:56:49
Nakuombea πŸ™
G
Grace Mushi2022-02-19 10:42:50
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
D
David Nyerere2021-12-05 22:19:18
Neema ya Mungu inatosha kwako
A
Ann Awino2021-09-15 03:14:29
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
R
Ruth Mtangi2021-08-03 17:25:12
Neema na amani iwe nawe.
C
Chris Okello2021-06-08 16:18:00
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu