Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Nifanye nini ili kuepuka kubakwa na mpenzi/ rafiki?

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Kuna baadhi ya vidokezo ambavyo vinaweza kukusaidia: 1. Usikae faragha na mwenzi wako kabla hujawa tayari na kumwamini. Ongozana na marafiki wengine hasa mwanzoni mwa urafiki wenu. Msitoke tu nyie wawili hadi hapo utakapojisikia kuwa umemjua kiasi cha kumwelewa na kumwamini. Pia jiepushe kukaa sehemu za faragha naye. 2. Kama utatoka naye, hakikisha kuwa kuna mtu anayejua mnakokwenda na ni muda gani unakusudia kurudi nyumbani. Ikiwezekana kuwa na namba ya simu ya mmoja kati ya rafiki zako. Hii itakusaidia kama ikijitokeza hali ya kutaka msaada. 3. Usikubali yeye alipe gharama zote. Ni vizuri kugawa gharama hizo kati yenu. Kama mtakwenda kwenye tamasha au kupata kinywaji hakikisha kulipia nusu ya hizo gharama. Ukifanya hivyo utamzuia mwenzio mawazo ya kukufikiria β€œkuwa anakudai ngonoβ€œ kama malipo ya pesa yake aliyotumia. 4. Ni vizuri kutafakari na kuweka kichwani kabla ya kwenda naye popote juu ya nini unachotaka na kile usichotaka kitokee. 5. Onyesha wazi kuwa unaposema β€œhapanaβ€œ unamaanisha β€œhapanaβ€œ usimpe nafasi ya kuchukulia hiyo β€œhapanaβ€œ kuwa ndiyo. 6. Amini hisia zako. Kama unaona unalazimishwa usisite kueleza maoni yako / unavyojisikia. Ikibidi ondoka sehemu hiyo.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! πŸ“

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About