Jinsi ya kutumia Kondomu

✍️ SW - Melkisedeck ShineπŸ“… 2022-04-16 18:44:21πŸ’¬ 0 comments⏱️ ~1 min read
πŸ“„ PDF

Wakati wa kutumia kondomu ya kiume ni muhimu kufuata hatua zifuatazo. Hakikisha kwamba pakiti inayoihifadhi haijapasuka na kwamba tarehe ya kuisha muda wake haijafika.
Uume ukishadinda, fungua pakiti kwa uangalifu. Minya sehemu ya juu kutoa hewa ndani ya kondomu wakati wa kuvalisha uume, ili kuzuia kupasuka kwa kondomu wakati wa kujamiiana. Visha uume kondomu taratibu mpaka uufunike wote. Ukiwa na uhakika kwamba kondomu imevishwa inavyotakiwa, unaweza kukutana kimwili na mwanamke.
Wakati wa kutoa uume kutoka ukeni, uwe mwangalifu kwamba kondomu bado ipo sehemu inayopaswa kuwa. Baada ya kutoa uume kutoka ukeni, vua kondomu kwa uangalifu uume ukiwa bado umedinda, ili kuepuka shahawa zisimwagikie ukeni. Tupa kondomu iliyotumika kwenye choo cha shimo au uichome. Usitupe kondomu iliyotumika ovyo. Pia usitupe kondomu iliyotumika kwenye vyoo vya kisasa yaani vya kuflashi na maji.
Ukinunua β€œsalama kondomuβ€œ ndani ya pakiti, kuna maelekezo kuhusu matumizi ya kondom. Unapotaka kutumia kondom wakati wa kujamiiana, ni vizuri ukajaribisha kwanza ukiwa peke yako ili kuzoea jinsi ya kuitumia.

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

0 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
No comments yet.