Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Haki za ujinsia na afya ya uzazi zinamhusu pia mtu anayeishi na ualbino?

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Haki za msingi; hasa zile zinazohusiana na kuthaminiwa na
kuheshimiwa kama binadamu zinawahusu binadamu wote
kuanzia siku unayozaliwa. Mataifa yote Ulimwenguni yameridhia
mikataba ya Kimataifa inayokubaliana na matamko haya ya
haki. Haki hizi ziko dhahiri katika sheria za nchi husika. Haki
muhimu za ujinsia na afya ya uzazi ni hizi:
β€’ Kupata habari juu ya ujinsia na mada zinazohusu afya ya
uzazi.
β€’ Mwanamke au mwanaume kuamua kwa uhuru na kuwajibika,
kama anataka kujamiiana lini na mtu gani.

β€’ Kuamua idadi ya watoto anaotaka kuzaa na hao watoto
wapishane miaka mingapi.
β€’ Kupata huduma za afya ya uzazi.
β€’ Kuamua bila kulazimishwa nani wa kufunga naye ndoa.
β€’ Kulindwa dhidi ya mila zenye madhara kama vile ukeketaji
wa wanawake.
Watu wote wakiwemo wale wanaoishi na ualbino au ulemavu
wa aina yoyote wanalindwa na haki za binadamu. Changamoto
iliyopo ni kwa wale watu wanaoishi na ualbino kutoa sauti katika
kutetea na kuhamasisha jamii juu ya haki zao.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! πŸ“

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About