Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/mobile/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Njia bora za kumfanya mtu aache kuvuta sigara

Featured Image

Ni kazi ngumu kidogo kuacha uvutaji wa sigara. Uvutaji ni tishio kwa maisha yetu. Yawezekana hufahamu kwamba nusu ya watu wanaovuta sigara watakufa, ikiwa ni matokeo ya athari kilevi hicho. Sigara inasababisha robo ya vifo vyote vya kansa nchini Uingereza kila mwaka.

Kuacha uvutaji sio jambo rahisi sana. Hii ndiyo sababu kwa nini hadi sasa bado kuna watu milioni 10 wanaovuta sigara nchini Uingereza. Huku watu kati ya milioni tatu hadi nne wanajaribu kuacha wakati wowote bila ya mafanikio.

Njia tofauti zinazowezesha kuacha matumizi ya kilevi hicho ni zifuatazo, kama zinavyotambuliwa kwa majina yafuatayo:

1. Cold turkey

Ni njia ya kujikatalia kuvuta sigara.

Mvutaji anatakiwa aishi na kanuni ya 'angalau mvuto mmoja.' Kwa mujibu wa wataalamu hao, hamu ya kawaida ya sigara inadumu kwa mtu walau kwa takribani dakika tano.

Hivyo, mvutaji anatakiwa kuwa na orodha ya mikakati ndani ya dakika tano hizo kuvuruga hisia, iwapo hamu ya kuvuta itakapomjia.

2. Tembe za kumungโ€™unya(Patches, gum, lozenges)

Kutumia tembe za kumungโ€™unya kwa wiki nane yaweza kuongezea mara mbili nafasi ya kuacha sigara. Itapunguzia tamaa ya kuvuta sigara, bila ya kuharibu afya binafsi. Inafanya kazi kwa kuchukua nafasi ya nikotini ipatikanayo kutoka kwenye sigara au tumbaku.
Ni lazima kufwata masharti utakayopewa na dakitari kabla na wakati wa kutumia dawa hizi

3. Sigara ya kielektroniki (Vape)

Watu wengi wamegeukia uamuzi wa kuacha sigara, kwa kuvuta sigara za kielektroniki ambazo kimsingi zimeumbwa mfano wa sigara haliso na zinazopatikana katika aina zote za miundo na ladha. Hivyo, ni rahisi kupata picha, kwa nini Waingereza wapatao milioni 2.9 wanaitumia.

Aina hiyo ya sigara, huifanya mikono ya mvutaji iwe na shughuli ya kufanya kwa kuvuta aina hiyo ya sigara isiyo na majivu na gesi chafu ya ya aina ya carbon monoxide au vingine vinavyopatikana katika sigara halisi.

Hata hivyo, tafiti kadhaa zinaonyesha hewa hiyo inaweza kusababisha mabadiliko ya chembehai zinazoweza kusababisha kansa.

Hayo ni matokeo ya tafiti mpya, ambayo yanaelezwa hayana ushahidi unaojitosheleza , jambo linaloleta hoja nyingine kwamba โ€˜vapeโ€™ inatakiwa kuvutwa kwa tahadhari.

4. Ushawishi kitaalamu (Hypnotism)

Utafiti uliofanywa kwa watu 6,000 wanaovuta sigara, inaonyesha kuwa njia hiyo ina mafanikio makubwa, kwa kuwashawishi wavutaji watambue madhara na faida za kuacha sigara

"Inachukua siku chache tu kwa nikotini kuondoka mwilini mwako. Kwa hiyo, kile unachoachwa nacho ni tamaa ya kisaikolojia," anasema mtaalamu Brian Jacobs, anayesema kinachoshughulikiwa hapo ni tamaa, wakati mtu yupo mapumzikoni.

Baada sigara ya mwisho

Baada ya saa nane, oksijeni hurudi katika hali ya kawaida mwilini na tindikali ya nikotini na hewa ya carbon monoxide hupungua kwa kiwango cha nusu ya kilichokuwapo.

Baada ya saa 48, mwilini mwa binadamu hakuna nikotini inayobaki mwilini na uwezo wa kuonja na harufu unaboreshwa. Hatari ya kuwa na mashambulizi ya moyo, nayo inaanza kupungua.

Hatua inayofuata baada ya kati ya wiki mbili na 12, mzunguko wa damu, hewa, maji na mahitaji mengine mwilini yanaboreka.

Ni hali inayoendelea hata kufika baada ya miezi mitatu hadi tisa, mapafu yanakuwa yameboreka kwa asilimia 10 na kukohoa kunakuwa kumepungua.

Inapofika mwaka mmoja umepita, hatari ya ugonjwa wa moyo kwa mvutaji inakuwa katika kiwango cha nusu ilivyokuwa awali na ikiendelea katika miaka 10 baadaye, hatari ya saratani ya mapafu huwa nusu kwa mvutaji, kulinganisha na alivyokuwa awali.

Ikiendelea baada ya miaka 15, moyo unakuwa salama dhidi ya hatari ya mashambulizi ya sawa na kuwa sawa na asiyetumia sigara.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Umuhimu wa kupata chanjo

Umuhimu wa kupata chanjo

Siku zote sisi wanadamu huwa tunaambizana kuwa, kinga ni bora kuliko tiba, tukiwa na maana kwamba... Read More

Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza

Vyakula vinavyofaa kutumiwa kwa mtu mwenye kisukari aina ya kwanza

Vyakula hivyo ni;

  1. Maharage
  2. Nyanya
  3. Samaki
  4. Mboga za majani zenye... Read More
Sababu ya meno kubadilika rangi

Sababu ya meno kubadilika rangi

Wapo baadhi ya watu wanashindwa hata kuachia kicheko chenye bashasha hii ni kwa sababu meno yao y... Read More

Tabia 10 zinazoweza kuharibu figo

Tabia 10 zinazoweza kuharibu figo

1.Kubana mkojo kwa muda mrefu
2.Kutokunywa maji ya kutosha kila siku
3.Kutumia chumvi n... Read More

Namna ya kujitibu chunusi kwa kutumia dawa ya meno au dawa ya mswaki

Namna ya kujitibu chunusi kwa kutumia dawa ya meno au dawa ya mswaki

Dawa ya mswaki au dawa ya meno ni dawa nyingine ya asili unayoweza kutumia kujitibu chunusi. Hii... Read More

Utajuaje kama una upungufu wa maji mwilini? Dalili ni hizi

Utajuaje kama una upungufu wa maji mwilini? Dalili ni hizi

Upungufu wa maji ni pale mwili unapopoteza kiasi kingi cha maji kwa njia mbalimbali, ikiwemo jasho n... Read More
Ushauri kuhusu mwili wako

Ushauri kuhusu mwili wako

Nimekutana na hiki kitabu japo nimekipitia juu juu nikaona nisiwe mchoyo Wa kukushirikisha wewe u... Read More

Matumizi ya karoti na asali kutibu presha ya kushuka

Matumizi ya karoti na asali kutibu presha ya kushuka

Hatua za kufuata

1. Tengeneza glasi moja ya juisi ya karoti

2. ... Read More

PROSTATE GLAND (TEZI DUME) TATIZO SUGU KWA WANAUME

PROSTATE GLAND (TEZI DUME) TATIZO SUGU KWA WANAUME

-Hii ni tezi ya wanaume yenye sifa zifuatazo.
~Ina umbo km yai(oval shape)
~Ina ukubwa ... Read More

Faida 25 za kutembea kwa Miguu

Faida 25 za kutembea kwa Miguu

Maendeleo ya sayansi na teknolojia yamebadili mfumo wa maisha ya watu pamoja na kuathiri afya zao kw... Read More
Ulaji mzuri hupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la chini la damu

Ulaji mzuri hupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la chini la damu

Ni mhimu kula mlo kamili kila siku. Kula lishe duni kunaweza kupelekea kuzalishwa kwa damu isiyo ... Read More

Umuhimu wa kula fenesi kiafya

Umuhimu wa kula fenesi kiafya

Fenesi ni miongoni mwa matunda ya msimu yenye umbo la kipekee huku likiwa na ladha tamu isiyomith... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About