Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/mobile/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Featured Image
Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.Naomba sana Baba wee, baraka yako nipokee. Bikira safi, Ee Maria nisipotee nisimamie. Mlinzi mkuu malaika wee kwa Mungu wetu niombee,nitake nitende mema tu na mwisho nije kwako juu.Amina.

NIA NJEMA.

Kumueshimu Mungu wangu,namtolea roho yangu. Nifanye kazi nipumzike ,amri zake tu nishike. Wazo,neno,tendo lote namtolea Mungu pote Roho,Mwili chote changu. Pendo na uzima wangu. Mungu wangu nitampenda wala dhambi sitatenda. Jina lako nasifia,utakalo hutimia kwa utii navumili. Teso na matata pia,nipe Bwana neema zako, niongeze sifa yako.Amina.

SALA YA MATOLEO.

Ee Yesu kwa mikono ya Bikira Maria,na kwa maungano na sadaka yako kuu. Ninakutolea sala,matendo,masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu ufalme wako utufikie.Amina.

BABA YETU.

Baba yetu uliye mbinguni,jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike.Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku.Utusamehe makosa yetu,kama tunavyo wasamehe na sisi waliyo tukosea. Usitutie katika kishawishi,lakini utuopoe maovuni.Amina.

SALAMU MARIA.

Salamu Maria,umejaa neema Bwana yu nawe,umebarikiwa kuliko wanawake wote,na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu,utuombee sisi wakosefu sasa na saa ya kufa kwetu.Amina.

KANUNI YA IMANI.

Nasadiki kwa Mungu,Baba Mwenyezi,muumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu Mwanaye wa pekee,Bwana wetu aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu,akazaliwa na Bikira Maria,akateswa kwa mamlaka ya ponsyo Pilato,akasulibiwa, akafa,akazikwa,akashukia kuzimu siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi,toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,kanisa takatifu katoliki ushirika wa Watakatifu,maondoleo ya dhambi,ufufuko wa miili na uzima wa milele.Amina.

AMRI ZA MUNGU.

1.Ndimi Bwana Mungu wako,usiabudu miungu wengine. 2.Usilitaje bure jina la Mungu wako. 3.Shika kitakatifu siku ya Mungu. 4.Waheshimu Baba na Mama upate miaka mingi na heri duniani. 5.Usiue. 6.Usizini. 7.Usiibe. 8.Usiseme uwongo. 9.Usitamani mwanamke asiye mke wako. 10.Usitamani mali ya mtu mwingine.

AMRI ZA KANISA.

1.Hudhuria misa takatifu domonica na sikukuu zilizo amuliwa. 2.Funga siku ya jumatano ya majivu,usile nyama siku ya Ijumaa kuuu. 3.Ungama dhambi zako walau mara moja kwa mwaka. 4.Pokea Ekarist takatifu hasa wakati wa Pasaka 5.Saidia kanisa katoliki kwa zaka. 6.Shika sheria katoliki za ndoa.

SALA YA IMANI.

Mungu wangu,nasadiki maneno yote linayo sadiki na kufundisha kanisa katoliki la Roma kwani ndiwe uliye fumbuliwa hayo,wala hudanganyiki na wala hudanganyi.Amina.

SALA YA MATUMAINI.

Mungu wangu,natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu,neema zako duniani na utukufu mbinguni.Kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi nawe mwamini.Amina.

SALA YA MAPENDO.

Mungu wangu,nakupenda zaidi ya chochote, kwani ndiwe mwema ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu kama nafisi yangu kwa ajiri yako.Amina.

SALA YA KUTUBU.

Mungu wangu,nimetubu sana dhambi zangu kwani ndiwe mwema,ndiwe mwenye kupendeza wachukizwa na dhambi. Basi sitaki kukosa tena nitafanya kitubio,naomba neema yako nipate kurudi.Amina.

SALA KWA MALAIKA MLINZI.

Malaika mlinzi wangu,unilinde katika hatari zote za Roho na za Mwili.Amina.

MALAIKA WA BWANA.

K.Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria. W.Naye akapata mimba kwa Roho mtakatifu. Salamu Maria….. K.Ndimi mtumishi wa Bwana. W.Nitendewe ulivyo nena. Salamu Maria….. K. Neno la Mungu akatwaa Mwili. W. Akakaa kwetu. Salamu Maria…. K. Utuombee Mzazi Mtakatifu wa Mungu. W. Tujaliwe ahadi za Kristu. Tuombe. Tunakuomba Ee Bwana utie neema yako mioyoni mwetu ili sisi tuliyojuwa kwa maelezo ya malaika kwamba, Kristu mwanao amejifanya mtu kwa mateso na msalaba wake. Tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu.Amina.

ATUKUZWE BABA.

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,kama mwanzo na sasa na siku zote na milele.Amina. K. Moyo Mtakatifu wa Yesu W.Utuhurumie. K. Moyo safi wa Bikira Maria. W. Utuombee. K. Mtakatifu Yosefu. W. Utuombee. K. Watakatifu somo wa majina yetu. W. Mtuombee. K.Watakatifu wote wa Mungu. W.Mtuombee. Kwa jina la Baba…..
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Victor Sokoine (Guest) on August 3, 2017

Tumaini ni nanga ya roho

Lydia Mzindakaya (Guest) on July 16, 2017

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

George Wanjala (Guest) on July 4, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Janet Wambura (Guest) on May 28, 2017

πŸ™πŸ™πŸ™

Monica Adhiambo (Guest) on April 29, 2017

Sifa kwa Bwana!

Peter Mbise (Guest) on March 30, 2017

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Bernard Oduor (Guest) on February 8, 2017

Mungu ni mwema, wakati wote!

Patrick Kidata (Guest) on December 19, 2016

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

George Tenga (Guest) on November 11, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Anthony Kariuki (Guest) on October 29, 2016

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Alex Nakitare (Guest) on October 2, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Andrew Mchome (Guest) on September 10, 2016

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Lydia Mahiga (Guest) on August 16, 2016

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Sharon Kibiru (Guest) on June 29, 2016

Mwamini katika mpango wake.

Isaac Kiptoo (Guest) on April 14, 2016

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Susan Wangari (Guest) on April 5, 2016

Neema ya Mungu inatosha kwako

Lucy Kimotho (Guest) on March 20, 2016

Dumu katika Bwana.

Stephen Mushi (Guest) on December 11, 2015

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Paul Ndomba (Guest) on October 7, 2015

πŸ™πŸ™πŸ™

Lucy Mushi (Guest) on July 19, 2015

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Joseph Kawawa (Guest) on June 7, 2015

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Victor Kamau (Guest) on May 27, 2015

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Peter Mugendi (Guest) on May 27, 2015

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Related Posts

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………β... Read More

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaok... Read More

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU KWA SIKU ZOTE TISA

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU KWA SIKU ZOTE TISA

Ufuatao ni mtiririko wa Novena ya Roho Mtakatifu kwa siku zote tisa.

Kusali nov... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makun... Read More

Majitoleo kwa Bikira Maria

Majitoleo kwa Bikira Maria

(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na... Read More

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkinga... Read More

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

SALA YA KUMWOMBA MT. YOSEFU MSAADA (SALA KUU KWA MTAKATIFU YOSEFU)

Ee Mt. Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu, na kisha omba shime ya Mchum... Read More

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About