Mafundisho kuhusu Neema

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-02-28 03:33:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF
Je, tunaweza kuhakikisha neema ya utakaso?
Hapana, hatuwezi kuhakikisha neema ya utakaso kwa kuwa ni tukio ambalo linapita maumbile na kufanyika rohoni, hivyo halifikiwi na hisi zetu. Pengine Mungu anatokeza dalili fulani za badiliko hilo kama vile furaha ya ndani au karama ya nje, lakini hizo hazihitajiki wala hazitoshi kuthibitishia mtu amepata neema hiyo.
β€œWengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu” (Math 7:22-23).
β€œNijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu” (1Kor 13:1-3).

Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)

Kuna aina ngapi za neema?
Kuna aina mbili za neema
1. Neema ya utakaso 2. Neema ya msaada

Neema ya Utakaso ni nini?
Neema ya Utakaso ni uzima wa Kimungu unaomiminwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu. (Yoh 1:16, Yoh 3:3-5)

Neema ya Utakaso yapatikanaje?
Neema ya Utakaso yapatikana kwa; 1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo 2. Sakramenti ya Kitubio 3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
4. Yaongezwa kwa kupokea Sakramenti nyingine 5. Kwa Sala 6. Kwa Ibada Takatifu 7. Kwa matendo mema

Neema ya Utakaso yapoteaje?
Neema ya Utakaso yapotea kwa kutenda dhambi kubwa (dhambi ya mauti)

Kuna Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso?
Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso ni;-
1. Kupendwa na Mungu hapa duniani 2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa

Neema ya Msaada ni nini?
Neema ya Msaada ni msaada tupatao kwa Roho Mtakatifu kutuongezea nguvu Rohoni tutende mambo mema na tuepuke Mabaya

Neema ya Msaada yapatikanaje?
Neema ya Msaada yapatikana kwa kupokea Sakramenti, kusali, na kutenda mambo ya Ibada (Yoh 15:5, 1Tim 2:4)
πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

50 comment(s)
A
Anna Sumari2017-12-08 11:39:12
Nguvu hutoka kwa Bwana
A
Alice Mwikali2017-03-14 07:03:08
Mungu akubariki!
A
Alex Nyamweya2017-01-10 19:40:53
Sifa kwa Bwana!
J
John Kamande2016-10-16 11:18:40
Endelea kuwa na imani!
A
Anna Sumari2016-10-06 17:39:20
Imani inaweza kusogeza milima
M
Mercy Atieno2016-07-20 12:10:22
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
P
Philip Nyaga2016-06-19 17:26:11
Katika imani, yote yanawezekana
J
Joseph Kawawa2016-03-23 10:28:58
Dumu katika Bwana.
L
Lucy Mahiga2015-12-15 10:33:28
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
S
Samuel Were2015-09-13 05:46:16
Tumaini ni nanga ya roho