Siri ya Yesu: Mwangaza Wa Maisha

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-12-20 06:33:00πŸ’¬ 100 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Siri ni hii, Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza. Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu. Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu. Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Kujikabidhi Kwa Yesu Kristu Yeye Aliye Mwangaza Wa Maisha

Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza

Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu.
Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu.
Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Yesu Kristu ni mwangaza wa maisha yetu, akiwepo giza lote hutoweka.
Yesu akiwepo hakuna haja ya kufukuza giza bali giza litatoweka Lenyewe.

Unapomkaribisha Yesu katika maisha yako umekaribisha mwanga katika maisha yako na utashinda dhambi na uovu kwa kuwa Yesu aliye mwanga atavifutilia mbali.

Kikubwa ni kumkaribisha Yesu katika maisha yako na kumruhusu atawale Maisha yako na kila kitu katika maisha yako. Ukiweza kuachilia yote kwa Bwana Yesu na kumpa maisha yako basi utashinda uovu/dhambi. Vile unavyojiweka karibu na Yesu ndivyo unavyoshinda dhambi na uovu wote.

Kumkabidhi Yesu MaishaΒ ni Kuamua kuishi kulingana na Mafundisho yake, kuachilia yote katika maongozi yake, kumshirikisha Yesu kwenye kila kitu katika maisha yako na Kuwa mkweli na muwazi mbele ya Yesu katika kila kitu.

Unapomkabidhi Yesu Maisha yako na vyote ulivyonavyo yeye huyatakatifuza na kuyafanya yawe kama yanavyotakiwa kuwa kitakatifu.

Changamoto kubwa kwa Wakristu ni kushindwa kujiweka Mikononi mwa Yesu kwa kuachilia yote na kukabidhi yote kwake. Wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ubinafsi na uchu wa kusimama wenyewe. Wengine wanashindwa kwa sababu ya kukosa Imani. Hawana uhakika kwamba wanachokifanya wanakifanya kweli.

Lakini ukiweza kweli kumkabidhi Yesu Maisha yako, kila kitu kinakua sawa na utafanikiwa kwenye kila kitu. Utaanza kuona unashinda uovu na dhambi kulingana na vile unavyojikabidhi na kujiachilia kwa Yesu.

Anza leo kujikabidhi kwa yesu kwa kiasi kile unachoweza. Yesu anaelewa ubinadamu na madhaifu yetu. Atakusaidia. Hata kama kuna wakati unaweza kujikabidhi kwake na kisha unaanguka tena, yeye ni mwenye huruma na ni mwelewa haswa kuhusu hali yako, atakusaidia na kukuwezesha. Weka nia ya kujikabidhi kwake na kisha utaendelea kidogo kidogo mpaka utajikuta umejikabidhi mikononi kwake kabisa.

KUMBUKA:Β Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza, mwanga ukiwepo giza halibaki linaondoka. Hata siku moja Giza haliwezi kuuzidi mwanga

Uwe na Imani basi, Mtumainie Yesu Kristu atakushindia uovu.

Yesu ndiyo dawa ya uovu na dhambi, kila unapoanguka dhambini mkimbilie yeye naye atakusamehe na kukuwezesha kushinda dhambi na uovu. Usichoke, kila siku jaribu na kujaribu mpaka utashinda.

Nami nakuombea kwa Jina Takatifu la Yesu, Akushindie Uovu na dhambi

πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

100 comment(s)
L
Linda Karimi2020-01-29 05:17:01
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
A
Anna Malela2019-12-16 04:14:34
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
E
Elizabeth Mrope2019-09-26 21:04:35
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
J
Joy Wacera2019-07-24 09:02:44
Rehema hushinda hukumu
J
Joyce Aoko2019-06-27 18:30:47
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
C
Charles Mboje2019-05-27 19:34:17
Rehema hushinda hukumu
D
Diana Mallya2019-05-24 03:34:36
Rehema zake hudumu milele
C
Charles Mchome2019-05-01 15:36:46
Imani inaweza kusogeza milima
B
Benjamin Masanja2019-03-29 01:14:02
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
G
Grace Wairimu2019-03-18 08:36:58
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
S
Susan Wangari2019-03-09 17:27:24
Mungu akubariki!
F
Francis Mtangi2019-02-28 11:35:46
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
C
Charles Mrope2019-02-26 03:46:00
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
P
Peter Otieno2019-02-18 06:30:10
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
J
Josephine Nekesa2019-02-07 11:36:10
Wakati wa Mungu ni kamilifu
J
Joseph Mallya2018-12-15 10:50:35
Katika imani, yote yanawezekana
S
Stephen Amollo2018-10-15 09:18:38
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
D
Daniel Obura2018-09-23 06:54:20
Mungu akubariki!
R
Richard Mulwa2018-06-24 14:51:46
Tembea kwa imani, si kwa kuona
A
Alice Mwikali2018-06-07 08:58:15
Endelea kuwa na imani!