Mafundisho kuhusu Neema

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-02-28 03:33:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF
Je, tunaweza kuhakikisha neema ya utakaso?
Hapana, hatuwezi kuhakikisha neema ya utakaso kwa kuwa ni tukio ambalo linapita maumbile na kufanyika rohoni, hivyo halifikiwi na hisi zetu. Pengine Mungu anatokeza dalili fulani za badiliko hilo kama vile furaha ya ndani au karama ya nje, lakini hizo hazihitajiki wala hazitoshi kuthibitishia mtu amepata neema hiyo.
β€œWengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu” (Math 7:22-23).
β€œNijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu” (1Kor 13:1-3).

Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)

Kuna aina ngapi za neema?
Kuna aina mbili za neema
1. Neema ya utakaso 2. Neema ya msaada

Neema ya Utakaso ni nini?
Neema ya Utakaso ni uzima wa Kimungu unaomiminwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu. (Yoh 1:16, Yoh 3:3-5)

Neema ya Utakaso yapatikanaje?
Neema ya Utakaso yapatikana kwa; 1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo 2. Sakramenti ya Kitubio 3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
4. Yaongezwa kwa kupokea Sakramenti nyingine 5. Kwa Sala 6. Kwa Ibada Takatifu 7. Kwa matendo mema

Neema ya Utakaso yapoteaje?
Neema ya Utakaso yapotea kwa kutenda dhambi kubwa (dhambi ya mauti)

Kuna Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso?
Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso ni;-
1. Kupendwa na Mungu hapa duniani 2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa

Neema ya Msaada ni nini?
Neema ya Msaada ni msaada tupatao kwa Roho Mtakatifu kutuongezea nguvu Rohoni tutende mambo mema na tuepuke Mabaya

Neema ya Msaada yapatikanaje?
Neema ya Msaada yapatikana kwa kupokea Sakramenti, kusali, na kutenda mambo ya Ibada (Yoh 15:5, 1Tim 2:4)
πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

50 comment(s)
C
Christopher Oloo2021-05-16 09:19:18
Mungu ni mwema, wakati wote!
A
Anna Malela2021-05-03 21:56:08
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
M
Martin Otieno2021-04-21 19:14:14
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
S
Stephen Amollo2021-04-18 17:47:41
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
M
Monica Adhiambo2021-02-27 12:15:20
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
S
Samson Tibaijuka2021-02-23 16:19:54
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
R
Rose Waithera2020-10-28 22:36:12
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
N
Nancy Kawawa2020-10-08 17:26:28
Wakati wa Mungu ni kamilifu
E
Edwin Ndambuki2020-10-05 01:49:04
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
J
Jackson Makori2020-01-17 09:02:44
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
E
Elijah Mutua2019-10-29 03:38:00
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
M
Moses Mwita2019-10-17 04:29:23
Rehema hushinda hukumu
D
Diana Mallya2019-07-21 06:24:01
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
J
John Lissu2019-07-10 04:42:28
Tembea kwa imani, si kwa kuona
F
Frank Sokoine2019-04-01 14:29:07
Baraka kwako na familia yako.
V
Victor Kamau2018-11-01 23:35:10
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
H
Henry Sokoine2018-08-03 17:19:18
Rehema zake hudumu milele
C
Catherine Naliaka2018-07-27 22:08:13
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
V
Violet Mumo2018-04-04 14:16:55
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
J
James Mduma2018-01-08 12:10:04
Mwamini Bwana; anajua njia