Siri ya Yesu: Mwangaza Wa Maisha

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2017-12-20 06:33:00πŸ’¬ 100 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Siri ni hii, Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza. Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu. Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu. Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Kujikabidhi Kwa Yesu Kristu Yeye Aliye Mwangaza Wa Maisha

Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza

Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu.
Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu.
Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Yesu Kristu ni mwangaza wa maisha yetu, akiwepo giza lote hutoweka.
Yesu akiwepo hakuna haja ya kufukuza giza bali giza litatoweka Lenyewe.

Unapomkaribisha Yesu katika maisha yako umekaribisha mwanga katika maisha yako na utashinda dhambi na uovu kwa kuwa Yesu aliye mwanga atavifutilia mbali.

Kikubwa ni kumkaribisha Yesu katika maisha yako na kumruhusu atawale Maisha yako na kila kitu katika maisha yako. Ukiweza kuachilia yote kwa Bwana Yesu na kumpa maisha yako basi utashinda uovu/dhambi. Vile unavyojiweka karibu na Yesu ndivyo unavyoshinda dhambi na uovu wote.

Kumkabidhi Yesu MaishaΒ ni Kuamua kuishi kulingana na Mafundisho yake, kuachilia yote katika maongozi yake, kumshirikisha Yesu kwenye kila kitu katika maisha yako na Kuwa mkweli na muwazi mbele ya Yesu katika kila kitu.

Unapomkabidhi Yesu Maisha yako na vyote ulivyonavyo yeye huyatakatifuza na kuyafanya yawe kama yanavyotakiwa kuwa kitakatifu.

Changamoto kubwa kwa Wakristu ni kushindwa kujiweka Mikononi mwa Yesu kwa kuachilia yote na kukabidhi yote kwake. Wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ubinafsi na uchu wa kusimama wenyewe. Wengine wanashindwa kwa sababu ya kukosa Imani. Hawana uhakika kwamba wanachokifanya wanakifanya kweli.

Lakini ukiweza kweli kumkabidhi Yesu Maisha yako, kila kitu kinakua sawa na utafanikiwa kwenye kila kitu. Utaanza kuona unashinda uovu na dhambi kulingana na vile unavyojikabidhi na kujiachilia kwa Yesu.

Anza leo kujikabidhi kwa yesu kwa kiasi kile unachoweza. Yesu anaelewa ubinadamu na madhaifu yetu. Atakusaidia. Hata kama kuna wakati unaweza kujikabidhi kwake na kisha unaanguka tena, yeye ni mwenye huruma na ni mwelewa haswa kuhusu hali yako, atakusaidia na kukuwezesha. Weka nia ya kujikabidhi kwake na kisha utaendelea kidogo kidogo mpaka utajikuta umejikabidhi mikononi kwake kabisa.

KUMBUKA:Β Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza, mwanga ukiwepo giza halibaki linaondoka. Hata siku moja Giza haliwezi kuuzidi mwanga

Uwe na Imani basi, Mtumainie Yesu Kristu atakushindia uovu.

Yesu ndiyo dawa ya uovu na dhambi, kila unapoanguka dhambini mkimbilie yeye naye atakusamehe na kukuwezesha kushinda dhambi na uovu. Usichoke, kila siku jaribu na kujaribu mpaka utashinda.

Nami nakuombea kwa Jina Takatifu la Yesu, Akushindie Uovu na dhambi

πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

100 comment(s)
M
Margaret Mahiga2022-09-21 07:28:52
Kwa Mungu, yote yanawezekana
K
Kenneth Murithi2022-06-18 17:12:00
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
E
Elizabeth Mtei2022-03-27 13:41:30
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
G
Grace Wairimu2022-02-13 21:53:11
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
G
Grace Mligo2021-12-10 09:36:42
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
A
Alex Nakitare2021-10-03 09:19:13
Mwamini Bwana; anajua njia
R
Raphael Okoth2021-09-21 14:08:39
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
J
Janet Sumaye2021-09-05 18:47:18
Nguvu hutoka kwa Bwana
J
Joseph Njoroge2021-07-30 22:16:31
Neema ya Mungu inatosha kwako
F
Francis Mtangi2021-07-12 22:36:42
Mungu ni mwema, wakati wote!
A
Agnes Njeri2021-02-06 02:18:30
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
R
Ruth Mtangi2021-02-05 01:10:34
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
L
Lucy Mahiga2020-12-30 03:31:46
Nakuombea πŸ™
V
Victor Kimario2020-12-25 18:03:20
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
L
Linda Karimi2020-06-15 18:56:47
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
A
Alice Wanjiru2020-05-10 10:30:16
Neema na amani iwe nawe.
E
Elizabeth Mrope2020-04-20 23:24:29
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
L
Lucy Mushi2020-03-07 22:14:47
Dumu katika Bwana.
D
David Musyoka2020-02-15 16:41:14
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
D
Dorothy Mwakalindile2020-02-10 18:47:58
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi