Amri za Kanisa: Mambo ya Muhimu kujua na Kuzingatia

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2016-12-19 17:34:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~2 min read
πŸ“„ PDF

Amri za Kanisa ni zipi?

Amri za kanisa ni;
1. Hudhuria Misa Takatifu Dominika na sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu
3.Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka
5. Saidia Kanisa Katoliki kwa zaka
6. Shika sheria Katoliki za ndoa.


Katika Amri ya kwanza ya Kanisa tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusikilize Misa kila siku ya Mungu na Sikukuu zilizoamriwa.


Sikukuu zilizoamriwa ni zipi?

Ndizo:

1. Kuzaliwa kwa YesuΒ - Noeli tarehe 25/12
2. Pasaka -Β Ufufuko wa Bwana Yesu
3. Kupaa Yesu β€”- Siku 40 baada ya Pasaka.
4. Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria 15/8
5. Sikukuu ya Watakatifu Wote 1/11


Katika Amri ya Kwanza ya kanisa tumekatazwa nini?

Tumekatazwa;
1. Kukosa Misa
2. Kufanya kazi nzito siku hizo


Kujinyima ni nini?

Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.


Nani ana lazima ya kufunga?

Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula. (Jumatano ya Majivu)


Siku za kufunga ni zipi? Na siku gani tumekatazwa kula nyama?

Siku za kufunga ni Jumatano ya majivu, siku za Kwaresima isipokuwa Dominika zake, na siku iliyokatazwa kula nyama ni siku ya Ijumaa kuu.


Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tatu ya Kanisa tumeamriwa kuungama mara kwa mara walau mara moja kila mwaka


Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Nne ya Kanisa tumeamriwa tupokee Ekaristi Takatifu walau mara moja kwa mwaka wakati wa pasaka.


Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa nini?

Katika Amri ya Tano ya Kanisa tumeamriwa kufahamu kuwa gharama za dini na za mapadre zatupasa. Yaanai wakristo walitegemeze Kanisa na wahudumu wake na hasa katika kazi ya kueneza injili.


Zaka ni nini?

Zaka ni asilimia kumi (10%) ya pato la mtu kwa mwaka ambalo anapaswa kulitoa kwa Kanisa.


Asiyelipa Zaka na michango mingine ya Kanisa ya lazima atenda dhambi gani?

Atenda dhambi kubwa: Yampasa kulipa na kuungama.


Amri ya Sita ya Kanisa Inadai nini?

Inadai kushika Sheria Takatifu Za ndoa

πŸ’¬

Discussion

Comments are public to read. Sign in to participate in the discussion.

50 comment(s)
πŸ” Login required to comment or reply

You can read the discussion, but only logged-in AckySHINE users can post comments or replies.

Log in to participate
L
Linda Karimi2020-09-24 21:43:36
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
D
David Chacha2020-07-13 05:20:07
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
B
Benjamin Masanja2020-07-10 07:11:05
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
A
Anna Mahiga2020-06-07 15:20:14
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
S
Samuel Omondi2020-03-17 18:59:29
Rehema zake hudumu milele
A
Andrew Mchome2019-11-24 03:23:23
Mwamini katika mpango wake.
S
Susan Wangari2019-11-04 08:53:05
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
P
Peter Otieno2019-03-14 13:12:12
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
A
Alice Wanjiru2019-02-04 14:02:56
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
L
Lydia Mzindakaya2019-01-29 23:04:22
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
S
Stephen Amollo2018-09-04 10:45:45
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
E
Edward Lowassa2018-08-13 12:42:57
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
A
Anna Malela2018-06-28 03:13:50
Nguvu hutoka kwa Bwana
N
Nancy Kawawa2018-04-05 17:48:40
Sifa kwa Bwana!
J
Joy Wacera2018-03-31 02:50:12
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
F
Francis Njeru2018-03-25 08:31:40
Imani inaweza kusogeza milima
M
Mariam Hassan2018-03-11 09:08:34
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
M
Moses Mwita2018-03-06 23:35:24
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
J
Jane Muthui2017-12-18 20:58:26
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
P
Peter Mwambui2016-12-01 16:37:41
Neema na amani iwe nawe.