Kilichowapata Watu 8 waliowahi kumdhihaki Mungu

✍️ DIN - Melkisedeck Leon ShineπŸ“… 2015-01-17 17:18:00πŸ’¬ 50 comments⏱️ ~3 min read
πŸ“„ PDF

1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)

Wakati alipokuwa akihojiwa na Mwandishi wa habari wa gazeti la #American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya #Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966.
Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata #MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)

Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la #Rio #De #Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema #Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute"
Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.

4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.

Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, Mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata #Mungu hawezi kuizamisha"
Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)

Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya
"Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'.
Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.

6. Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa Mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa Mama, huyo #Mungu labda akae kwenye boneti la gari".
Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa. Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.

7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)

Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya…kibaya na kibaya kama #Biblia"
Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)

Huyu alifuatwa na #Bill #Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simhitaji #Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu.

#share Ujumbe huu Kwa Ndugu na jamaa,ujumbe huu utawasidia kumuheshimu Mungu na kumtii.

Mungu ni pendo

πŸ’¬

Discussion

Share a thoughtful comment or reply. Content is escaped before display.

50 comment(s)
J
James Kimani2020-09-17 06:01:27
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
B
Brian Karanja2020-07-04 00:24:47
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
F
Francis Njeru2020-07-01 17:56:12
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
J
John Mwangi2020-03-07 00:37:50
Sifa kwa Bwana!
N
Nancy Komba2020-01-25 06:15:20
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
E
Elizabeth Malima2019-08-04 17:43:27
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
W
Wilson Ombati2019-06-07 14:05:03
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
V
Victor Kamau2019-06-02 23:56:11
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
M
Martin Otieno2019-05-31 23:55:32
Tembea kwa imani, si kwa kuona
J
Jacob Kiplangat2019-05-25 01:04:40
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
V
Violet Mumo2019-05-20 22:33:35
Wakati wa Mungu ni kamilifu
P
Philip Nyaga2019-01-21 08:56:53
Tumaini ni nanga ya roho
D
Diana Mumbua2019-01-09 11:54:44
Mwamini katika mpango wake.
S
Samuel Were2018-11-08 11:45:23
Kwa Mungu, yote yanawezekana
J
Janet Mwikali2018-07-16 12:54:45
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
S
Sharon Kibiru2018-07-09 19:46:09
Mungu akubariki!
F
Fredrick Mutiso2018-04-17 04:03:28
Endelea kuwa na imani!
M
Margaret Mahiga2018-01-05 12:31:53
Imani inaweza kusogeza milima
R
Rose Waithera2017-10-27 03:44:38
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
T
Thomas Mwakalindile2017-09-01 08:26:03
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini