Log in to access your menu with tools for managing ๐ tasks, ๐ฅ clients, ๐ฐ finances, ๐ learning, ๐ personal growth, and ๐ spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya makardinali na maaskofu wakuu; Uwape moyo wa kichungaji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wa majimbo; Uwajaze na Roho wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre watawa; Wakamilishe katika wito wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre walioko hatarini; Uwaokoe ee Bwana
Updated at: 2024-05-27 07:13:38 (2 years ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema Kwa ajili ya makardinali na maaskofu wakuu; Uwape moyo wa kichungaji ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wa majimbo; Uwajaze na Roho wako ee Bwana Kwa ajili ya mapadre watawa; Wakamilishe katika wito wao ee Bwana Kwa ajili ya mapadre walioko hatarini; Uwaokoe ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wenye udhaifu; Uwatie nguvu ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wenye hofu; Uwape amani ee Bwana Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; Uwavuvie upya ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wakaao upweke; Uwasindikize ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wamisionari; Uwalinde ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wanaohubiri; Uwaangazie ee Bwana Kwa ajili ya mapadre na watawa waliokufa; Uwafikishe kwenye utukufu wako ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie hekima na ufahamu wako ee Bwana Kwa ajili ya mapadre wote; Uwajalie elimu na shauri lako Kwa ajili ya mapadre wako; wajalie wakuheshimu na wakuogope Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie subira na upendo Kwa ajili ya mapadre wote; wajalie utii na upole Kwa ajili ya mapadre wote; uwajalie hamu kuu ya kuokoa roho za watu Kwa ajili ya mapadre wote; wape fadhila za imani, matumaini na mapendo Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie upendo mkuu kwa Ekaristi Tunakuomba uwajalie mapadre wote; Waheshimu uhai na hadhi ya mtu ee Bwana Tunakuomba uwajalie mapadre wote nguvu na bidii katika kazi zao ee Bwana Tunakuomba uwajalie mapadre wote amani katika mahangaiko yao ee Bwana Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Utatu Mtakatifu ee Bwana Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Bikira Maria ee Bwana Uwajalie mapadre wote wawe mwanga wa Kristo ee Bwana Uwajalie mapadre wote, wawe chumvi kwa ulimwengu ee Bwana Uwajalie mapadre wote, wajizoeze kujitoa sadaka na kujinyima ee Bwana Uwajalie mapadre wote, wawe watakatifu kimwili, kiakili na kiroho ee Bwana Uwajalie mapadre wote wawe watu wa sala ee Bwana Uwajalie mapadre wote wawe kioo cha imani kwako ee Bwana Uwajalie mapadre wote wajali sana wongofu wetu ee Bwana Uwajalie mapadre wote wawe waaminifu kwa wito wao wa kikuhani ee Bwana Uwajalie mapadre wote, ili mikono yao ibariki na kuponya ee Bwana Uwajalie mapadre wote wawake moto wa mapendo yako ee Bwana Uwajalie mapadre wote hatua zao zote ziwe kwa ajili ya utukufu wa Mungu ee Bwana Uwajalie mapadre wote wajazwe na Roho Mtakatifu na uwajalie karama zake kwa wingi ee Bwana.
Tuombe. Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, usikie sala tunazokutolea kwa ajili ya mapadre wetu. Uwajalie wafahamu waziwazi kazi uliyowaitia kuifanya, uwape neema zote wanazohitaji ili waitikie wito wako kwa ushujaa, kwa upendo, na majitoleo yenye udumifu katika mapenzi yako matakatifu. Amina.
Mungu wangu, natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristu, neema zako duniani na utukufu mbinguni, kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi, nawe mwamini. Amina
Updated at: 2024-05-27 07:14:19 (2 years ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.
Updated at: 2024-05-27 07:14:25 (2 years ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.
TUOMBE Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu, umetaka watu wako waokoke, ukamweka Malaika Mkuu Mikaeli kuwa Mkuu wa Kanisa lako, Utukinge na adui zetu, wasitusmbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako Mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana Wetu Yesu Kristo. Amina.
Utuombee Ee Mtukufu Mtakatifu Mikaeli Mkuu wa Kanisa la Yesu Kristo, tujaliwe ahadi za Kristo. Amina.