Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Maharage (beans 2 vikombe vya chai) Nazi (coconut milk kiasi) Vitunguu maji (onion 1kikubwa) Nyanya (fresh tomato 1) Kitunguu swaum (garlic paste 1/4 kijiko cha chai) Chumvi (salt kiasi) Curry powder 1 kijiko cha chai Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Chemsha maharage mpaka yaive kisha yaweke pembeni. Kaanga vitunguu maji na mafuta mpaka vianze kuwa vya brown kisha weka kitunguu swaum,nyanya na curry powder. kaanga mpaka nyanya iive kisha tia maharage na chumvi kiasi. Geuza mpaka mchanganyiko uchanganyike vizuri. Baada ya hapo tia tui la nazi na ukoroge vizuri na uache lichemke mpaka liive. Baada ya hapo ipua na maharage yatakuwa tayari kwa kuliwa
Updated at: 2024-05-25 10:34:46 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
1 kilo unga wa ngano 240 ml maji ya vugu vugu 2 olive oil kijiko kikubwa cha chakula 2 asali kijiko kidogo cha chai 1 chumvi kijiko kidogo cha chai 1 hamira ya chenga kijiko kidogo cha chai
JINSI YA KUPIKA
Chukua bakuli weka maji ya uvugu vugu, amira ya chenga, asali na chumvi kisha koroga ichanganyike vizuri acha itulie kwa dakika 10. Kisha chukua olive oil na unga wa ngao mimina kidogo kidogo changanya mpaka ichanganyike safi kabisa kisha anza kukanda kama mchanganyiko wa chapati au maandazi. Baada ya mchanganyiko wako kua mgumu safi kabisa funika bakuli lako na mfuko wa plastiki au cling film kwa muda wa saa 1 katika joto la chumba na mchanganyiko wako utaumuka baada ya muda huo. kisha ukandamize mchanganyiko huo wa unga na kua flati kama mwanzo. Kata mafungu matano hadi saba ya ujazo sawa inategemea na ukubwa wa piza unaopenda we mlaji kisha sukuma umbo la duara. Tengeneza mchuzi mzito wa nyanya kisha weka juu ya kitako cha piza na kuitandaza vizuri kwenye pizza yako kama unavyopaka siagi kwenye mkate. Usisahau kuweka chumvi na sukari kidogo katika mchuzi wa nyanya ili kukata uchachu. Katakata nyanya, kitunguu, pili pili hoho, na bilinganya na kuziweka juu ya pizza yako kwa mpangilio ukitanguliza biringanya, ikifuatiwa na pili pili hoho, kitunguu maji na nyanya. Kisha chukua mozarella cheese ikwaruze katika mkato mdogo rahisi kuyeyuka kwa kutumia kwaruzo la karoti linafaa. kisha chukua mkwaruzo wa mozarella cheese na unyunyizie juu ya hizo mboga. Weka pizza yako kwenye sahani ya bati au pizza pan ili isaidie kuiva upande wa chini. Weka pizza yako kwenye oven ambayo imeshawashwa na ina joto 400 - 450 F. Choma kwa dakika 20 hadi 25 iwe kaukau na rangi ya kahawia pia cheese itakua imyeyuka na kusambaa vizuri juu ya pizaa.
NB: Unaweza weka mchanganyiko wa nyama yeyote ile kama salami, nyama ya ngombe, nyama ya kuku au samaki kwa kufata maelekezo sawa sawa na hii piza ya mboga, tofauti yake itakua huweki mboga unaweka nyama.
Updated at: 2024-05-25 10:23:07 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 2 ½ gilasi
Sukari ¾ gilasi
Samli 1 gilasi
Mayai 2
Baking powder 2 kijiko vya chai
Vanilla 1 ½ kijiko cha chai
Maganda ya chungwa 1
MAPISHI
Tia kwenye machine ya kusagia (blender) mayai, sukari, vanilla, samli na maganda ya chungwa, saga vizuri. Tia unga kwenye bakuli pamoja na baking powder, mimina vitu ulivyosaga kwenye bakuli, changanya. Punguza unga uliochanganya kidogo weka pembeni. Unga uliobakia tia kwenya tray ya kuchomeya, utandaze vizuri, tia jam juu yake. Chukua la kukwaruzia carrot (grater) ukwaruze unga uliuopunguza juu ya jam. Choma kwa muda dakika 20 moto wa 180 C.
Acha ipowe kidogo, zikate vipande vya mraba (square) Tayari kwa kula.
Updated at: 2024-05-25 10:34:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIPIMO VYA SAMAKI
Samaki wa sea bass vipande - 1 1/2 LB (Ratili) Kitunguu saumu(thomu/galic) -1 Kijiko cha supu pilipili mbichi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chai Bizari ya manjano au ya pilau - 1/2 Kijiko cha chai Paprika ya unga au pilipili ya unga - 1 kijiko cha chai Chumvi - Kiasi Ndimu Mafuta - 3 Vijiko vya supu
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
Roweka samaki kwa viungo hivyo vyote kwa muda wa robo saa hivi.
Washa oven moto wa 400F. Kisha weka samaki katika trea na choma kwa muda wa dakika 15 na weka moto wa juu dakika za mwisho ili ipate rangi nzuri. Ikishaiva epua na itakuwa tayari kuliwa.
VIPIMO VYA MBOGA
Gwaru (green beans) - 1 LB Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 kijiko cha supu Karoti - 4-5 Chumvi - Kiasi Bizari ya manjano - 1/2 Kijiko cha chai Pilipili manga - 1/4 kijiko cha chai Mafuta ya zaituni - Kiasi
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
Kata kata karoti na toa sehemu ya mwisho za binzi. Weka mafuta katika sufuria kisha kaanga karoti na gwaru Kisha weka moto mdogo na funika ili ziwive na sio kuvurujika. Karibu na kuiiva tia thomu kaanga kidogo,tia bizari ,chumvi na pilipili manga. Ikisha changanyikana vizuri epua na tayari kuliwa na wali na samaki.
Updated at: 2024-05-25 10:23:14 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi - 15 takriiban
Nayma ya ng’ombe - 1 kilo
Kitunguu maji - 1
Nyanya - 3
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu
Tangawizi mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi ilopondwa - 2
Jira/cummin/bizari ya pilau ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Ndimu - 1
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama kwa ndimu, chumvi na tangawizi mbichi na kitunguu thomu. Menya ndizi na zikatekate vipande kiasi, weka katika sufuria. Katakata kitunguu na nyanya utie katika ndizi. Tia jira na chumvi. Nyama ikiwiva mimina pamoja na supu yake ufunike ndizi ziwive na kuwa tayari kuliwa. Ukipenda tia pilipili mbuzi zichemke pamoja na ndizi.
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga wa ngano vikombe vikubwa 3 Boga lililopondwa kikombe 1 Baking powder vijiko vidogo Sukari kikombe kikubwa 1 Blue band kikombe ½ Vanilla kijiko kidogo 1 Mayai 2 Maji kiasi/ maziwa (kama nilazima)
Hatua
• Osha boga, Kata, ondoa mbegu, kisha kata vipande vikubwa, chemsha na maji mpaka vilainike. • Kwangua boga la ndani ukiacha maganda na ponda sawasawa. • Chekecha unga (kila kikombe 1, vijiko vidogo 2 vya baking powder) kwenye bakuli kubwa. • Ongeza blue band na changanya sawasawa na vidole. • Ongeza sukari na changanya. • Ongeza mayai na koroga na mwiko. • Ongeza boga lililopondwa na koroga njia moja mpaka ilainike. • (Kama haikulainika ongeza yai /mayai au maziwa/ maji kidogo). • Ongeza vanilla na koroga. • Paka mafuta chombo cha kuokea au sufuria kisha chekecha unga kidogo wa ngano. • Mimina rojo la keki kwenye sufuria au chombo cha kuokea. • Oka kwenye oven au tumia sufuria na weka mkaa wa moto juu na chini moto kidogo mpaka iive. • Jaribu kuchoma kisu katikati, kama ni kavu keki imeiva, epua, pozesha kata tayari kwa kula, kama kitafunio.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi ulaya (baking potato 5 vya wastani) Parprika 1 kijiko cha chai Pilipili mtama ilyosagwa (ground black pepper 1 kijiko cha chai Kitunguu swaum cha unga (garlic powder 1 kijiko cha chai) Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil) Marination za samaki (angalia kwenye recipe ya samaki ya nyuma)
Matayarisho
Osha viazi na maganda yake kisha vikaushe na uvikate vipande vya wastani. Kwa kila kiazi toa vipande 6. Kisha vitie kwenye bakuli na utie parpika, pilipili mtama ya unga, kitunguu swaum cha unga, chumvi na mafuta kama vijiko 2 vya chakula. Changanya pamoja na kisha uvibake katika oven kwa muda wa dakika 25. Hakikisha vinakuwa rangi ya brown. Vikisha iva vitoe. Wamarinate samaki, na uwaoke kisha wasevu na potato wedges tayari kwa kuliwa (Jinsi ya kupika samaki, angalia katika recipe za nyuma)
Updated at: 2024-05-25 10:37:55 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Mashonanguo mkono 1 Tui la nazi kikombe 1 Karanga zilizosagwa kikombe ½ Mafuta vijiko vikubwa 4 Kitunguu 1 Nyanya ndogo 2 Chumvi kiasi
Hatua
• Chambua mashona nguo mateke, osha na katakata. • Menya osha na katakata kitunguu. • Osha, menya na katakata nyanya. • Kaanga karanga, ondoa maganda na saga zilainike. • Kuna nazi na chuja tui. • Kanga kitunguu, weka nyanya na koroga mpaka zilainike. • Weka mashona nguo na chumvi kisha koroga sawa sawa, funikiakwa dakika 5 -10. • Changanya tui la nazi na karanga, ongeza kwenye hizo mboga ukikoroga kwa dakika 5, punguza moto ili ziive taratibu. • Onja chumvi na pakua kama kitoweo. Uwezekano Changanya mnavu, mgagani, mashonanguo kidogo ki¬dogo au mboga nyingme. Tumia maziwa au krimu badala ya tui la nazi. Weka nyama au dagaa au samaki au mayai badala ya - karanga.
Jinsi ya kupika Pilau ya Mpunga Na Nyama Ya Ng’ombe
Updated at: 2024-05-25 10:23:15 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mpunga - 4 vikombe
Nyama - 1 kilo moja
Kitunguu maji - 3
Mbatata/viazi - 7 vidogodogo
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa 3 vijiko cha supu
Bizari nzima/ya pilau/uzile/cumin - 3 vijiko vya supu
Mdalasini - 3 vipande
Hiliki - 7 punje
Pilipili manga nzima - 1 kijiko cha supu
Chumvi kiasi
Mafuta - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele weka kando Katakataka vitunguu slice ndogo ndogo. Weka mafuta katika sufuria kisha ukaange vitunguu pamoja na mdalasini, hiliki pilipilimanga. Vitunguu vikigeuka rangi unatia kitunguu thomu na tangawizi. Tia supu kidogo na nyama, kisha tia bizari ya pilau/uzile, na viazi/mbatata. Maliza kutia supu yote, na ikiwa ni kidogo ongeze maji kiasi cha kuivisha mchele. kisha tia mchele ufunike hadi wali uwe tayari. Ikiwa unatumia mkaa palia juu yake, ikiwa hutumii uache uive kwa moto mdogo mdogo.
Updated at: 2024-05-25 10:23:05 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mayai yaliochemshwa 4 Nyama ya kusaga robo kilo Kitunguu swaum Tangawizi Limao Chumvi Pilipili Breadcrambs Carry powder Binzari nyembamba ya unga Yai moja bichi Mafuta
Matayarisho
Marinate nyama na pilipili, kitunguu swaum, tangawizi, limao, chumvi, carry powder, binzari nyembamba na breadcrambs pamoja. Kisha vunja yai moja bichi kwenye kibakuli na ulikoroge kisha tia kwenye mchanganyiko wa nyama.Gawanisha matonge manne kwa ajili ya kuzungushia kwenye mayai .Chemsha mayai kwa muda wa dakika 20. Yakisha iva acha yapoe na kisha yamenye maganda na uyaweke pembeni. Baada ya hapo chukua yai moja lililochemshwa na ulizungushie donge moja la mchanganyiko wa nyama. fanya hivyo kwa mayai yote yaliobakia. Baada ya hapo paka mafuta kwa nje ya hizo eggchop na kisha paka mafuta kwenye sinia la kuokea na uziokee kwenye oven kwa moto wa kawaida, kwa muda wa dakika 20.Na eggchop zako zitakuwa tayari kwa kuliwa