Log in to access your menu with tools for managing π tasks, π₯ clients, π° finances, π learning, π personal growth, and π spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:46 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi laini (Matoke 6) Viazi mbatata (potato 3) Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2) Kitunguu swaum (garlic 6 cloves) Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo) Vitunguu (onion 1) Pilipili (chilli 1 nzima) Chumvi (salt to your taste) Mafuta (vegetable oil) Limao (lemon 1/2) Curry powder (1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo) Mchele (rice 1/2 kilo) Vitunguu (onion 2) Viazi (potato 2) Vitunguu swaum (garlic 3 cloves) Tangawizi (ginger) Nyanya ya kopo (tomato 1/2 ya tin) Curry powder (1/2 kijiko cha chai) Binzari nyembamba ya kusaga (cumin 1/2 kijiko cha chai) Binzari manjano (tarmaric 1/2 kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Chumvi (salt) Rangi ya chakula (food colour) Giligilani (fresh coriander) Maziwa ya mgando (yogurt kikombe 1 cha chai) Hiliki nzima (cardamon 3cloves) Karafuu (clove 3) Pilipili mtama nzima (black pepper 5) Amdalasini (cinamon stick 1)
Matayarisho
Katakata nyama kisha ioshe na uiweke kwenye sufuria kisha tia kitunguu swaum, tangawizi, nyanya, curry powder, binzari zote, chumvi na maziwa ya mgando kisha bandika jikoni ichemke mpaka nyama iive na mchuzi ubakie kidogo.Baada ya hapo kaanga viazi na uweke pembeni, kisha kaanga vitunguu na mafuta mpaka viwe ya brown na kisha uvitie viazi vitunguu, na mafuta yake katika nyama. Koroga na uache uchemke kidogo kisha ipua na utie fresh coriander iliyokatwa na hapo mchuzi wako utakuwa tayari. Baada ya hapo loweka mchele wako kwa muda wa dakika 10, kisha chemsha maji yatie chumvi, hiliki, karafuu, pilipili mtama na abdalasin na mafuta. Yakisha chemka tia mchele na uache uchemke mpaka ukauke maji yakisha kauka tia rangi ya chakula na uanze kugeuza ili ichanganyike na wali wote. Baada ya hapo ufunike na uache mpaka uive. Na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga 300gm
Siagi 225gm
Icing Sugar 60gm
Chokoleti iliyokoza (Dark Chocolate) - 225gm
Vanilla β Vijiko 2 vya chai
Yai -1
Baking Powder Β½ kijiko cha chai
Njugu za vipande Β½ kikombe cha chai
Njugu zilizosagwa ΒΌ kikombe cha chai
JINSI YA KUTAYARISHA
Piga sukari na siagi katika mashine ya keki mpaka iwe laini Kisha mimina yai na vanilla koroga vizuri Mwisho mimina unga na baking powder polepole mpaka ichanganyike. Kata kata umbo (shape) lolote unavyopenda (kama nyota, pembetatu,duara, kopa n.k) Panga kwenye treya na choma kwa moto wa 350Β°C , vikibadilika rangi kidogo tu vitoe Yayusha chokoleti tia kwenye bakuli ndogo. kisha paka kwa kijiko au chovyea upande mmoja mmoja wa biskuti kisha nyunyizia njugu za kipande na njugu ya unga. Panga kwenye sahani tiyari kunywewa na chai ya maziwa au kahawa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Mchele - 3 vikombe
Nyama ya kusaga - 1 LB
Mchanganyiko wa Nafaka upendazo; maharagwe, njegere, mbaazi n.k 1 mug
Vitunguu maji kata vipande vipande - 3 vya kiasi
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 vijiko vya supu
Mafuta - Β½ Kikombe
Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) - 2 vijiko vya chai
Vipande vya supu (Maggi cubes) - 3
Maji (inategemea mchele) - 5
Chumvi - Kiasi
MAPISHI
Osha mchele na roweka. Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown. Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo. Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive. Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo. Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo. Tia mchele, koroga kidogo. Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida) *Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15. *Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil. Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Filigisi (chicken gizzard) 1/2 kilo Carrot iliyokwanguliwa 1 Nyanya 1/2 kopo Vitunguu maji 1 kikubwa Tangawizi/swaum 1 kijiko cha chai Hoho 1 iliyokatwakatwa Limao 1/2 Chumvi Curry powder 1/2 kijiko cha chai Turmaric 1/2 kijiko cha chai Chilli powder 1/4 kijiko cha chai Mafuta Chopped coriander
Matayarisho
Safisha filigisi kisha zikate vipande vidogo vidogo.Zichemshe pamoja na chumvi, limao na nusu ya tangawizi na swaum mpaka ziive (hakikisha unabakiza supu kidogo). Baada ya hapo kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia tangawizi na swaum iliyobakia na kaanga kidogo kisha tia nyanya. Zipike mpaka ziive kisha tia spice zote pamoja na chilli. Zipike kidogo kisha tia filigisi (bila supu kwanza) Zichanganye vizuri na uzipike kidogo. Baada ya hapo tia carrot na hoho na supu iliyobakia. Vipike pamoja mpaka viive na supu ibakie kidogo sana. Malizia kwa kutia coriander na uipue na hapo firigisi zako zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora
ππ₯¦π₯β¨π§π¦π½οΈ Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora! ππ²π Njoo, tujifunze jinsi ya kuandaa mlo mzuri kwa watoto wako! π½οΈβ¨π§π¦π Tembelea makala yetu sasa! ππ«#AfyaKwaWatoto #LisheBora #MloMzuri #TunzaWatoto #ZaidiKwenyeMakalaYetu
Updated at: 2024-05-25 10:22:23 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Upishi wa Afya kwa Watoto: Milo Mzuri na Lishe Bora ππ₯¦
Habari za leo wapendwa wasomaji! Leo nataka kuzungumzia kuhusu umuhimu wa upishi wa afya kwa watoto. Kama AckySHINE, ninalo jukumu la kusaidia kila mtu kupata lishe bora na kuishi maisha yenye afya tele. Kwa hivyo, leo nitalenga katika upishi wa afya kwa watoto na umuhimu wa milo mzuri na lishe bora.
Milo mzuri ni muhimu sana kwa watoto kwani hutoa nishati wanayoihitaji kwa shughuli zao za kila siku. Kwa mfano, mlo mzuri unaweza kuwa na ugali, maharage, samaki, na mboga mboga kama karoti, pilipili, na mchicha.
Lishe bora ni msingi wa ukuaji na maendeleo ya mtoto. Kwa kuwapa watoto lishe bora, tunajenga mwili wenye nguvu na mfumo wa kinga imara.
Matunda na mboga mboga ni mhimu sana katika upishi wa afya kwa watoto. Matunda kama ndizi, machungwa, na embe hutoa vitamini na madini muhimu kwa miili yao. Mboga mboga kama karoti, kabichi, na spinach zinaongeza nyuzi, vitamini, na madini muhimu.
Kwa kuwa watoto hupenda vitafunwa, tumia wakati mzuri kuwapa vitafunwa vyenye afya kama vile karanga, parachichi, na tambi za mchele. Vitafunwa hivi vina lishe bora na hutoa nishati kwa watoto wetu.
Kama AckySHINE, napendekeza kuwa na milo ya kawaida na kufanya kila mlo kuwa wa kufurahisha na wa kuvutia kwa watoto. Unaweza kujaribu kutengeneza milo yenye rangi mbalimbali ili kuwavutia watoto kula na kufurahia chakula chao.
Kwa watoto ambao hawapendi mboga mboga, unaweza kujaribu kuzipika kwa njia tofauti ili kuongeza ladha na kufanya ziwe za kuvutia kwa mtoto wako. Kwa mfano, unaweza kuzikaanga mboga mboga kwenye mafuta kidogo na kuongeza viungo vinavyopendwa na mtoto wako.
Pia, ni muhimu kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata protini ya kutosha katika milo yao. Protini husaidia katika ukuaji wa misuli na kuboresha afya ya ngozi. Unaweza kuwapa watoto wako nyama kama kuku au samaki, au hata maharage na karanga.
Kama mzazi, ni muhimu kuwa mfano mzuri kwa watoto wako. Kwa kuwa unakula lishe bora, watoto wako watafuata mfano wako na wataona kuwa ni kitu cha kawaida na muhimu.
Pia, hakikisha watoto wako wanakunywa maji ya kutosha. Maji ni muhimu katika kuweka mwili kuwa na afya. Badala ya vinywaji vyenye sukari, chagua maji safi na salama kwa watoto wako.
Ni vizuri kuwashirikisha watoto katika upishi. Wanaposhiriki katika maandalizi ya chakula, wanakuwa na hamu ya kula chakula hicho na wanafurahia kujaribu vitu vipya. Unaweza kuwapa majukumu kama vile kukata mboga au kuchanganya viungo.
Kama AckySHINE, napendekeza kutumia vyombo vya kuvutia na rangi mbalimbali katika kuwawekea watoto chakula chao. Hii itawavutia na kuwafanya wafurahie chakula chao.
Kumbuka kuwa kila mtoto ni tofauti, na wanaweza kuwa na upendeleo tofauti katika chakula. Sio kila mtoto atapenda vitu vyote. Jaribu kuelewa mapendezi ya mtoto wako na kujaribu kuwapa chakula wanachopenda, bila kusahau lishe bora.
Pia ni muhimu kuzungumza na watoto wako kuhusu umuhimu wa lishe bora na jinsi inavyowasaidia kuwa na afya bora. Eleza umuhimu wa matunda na mboga mboga na jinsi zinavyojenga miili yao.
Kuwa na ratiba ya milo na muda maalum wa kula pia ni muhimu. Hii itawasaidia watoto wako kuwa na mfumo mzuri wa chakula na kuzuia matumizi ya vyakula visivyo na lishe.
Mwisho lakini sio kwa umuhimu, nataka kusikia maoni yako. Je! Una mbinu yoyote ya kuwafanya watoto wako wapende kula chakula chenye lishe bora? Je! Unapika nini kwa watoto wako ili kuhakikisha wanapata milo mzuri? Na je! Unadhani upishi wa afya ni muhimu kwa watoto? Naamini kuwa tukiweka umuhimu katika upishi wa afya kwa watoto, tutaweza kuwajengea msingi imara wa afya na ustawi. Tafadhali shiriki maoni yako hapa chini! Asante sana na nakutakia siku njema! πππ₯¦
Updated at: 2024-05-25 10:23:06 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga vikombe 2
Sukari ya kusaga 1/4 Kikombe
Siagi 250 gms
Jam kisia
Ufuta kisia
Vanilla 1 kijiko cha chai
MAPISHI
Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai, sukari na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri. Tia baking powder, na unga na changanya kwa mkono vizuri. Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni. Tengeneza viduara vidogo vidogo. Bonyeza kila kiduara katikati kwa kidole, kisha weka jam, halafu juu yake paka mayai na unynyuzie ufuta. Pika katika moto wa chini 350ΒΊF kwa muda wa dakika 20-25. Tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:03 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi mbatata (potato 4 vya wastani) Nyama ya kusaga (mince beef 1 kikombe cha chai) Kitunguu (onion 1 cha wastani) Carrot 1 Hoho (green pepper 1/2) Kitunguu swaum (garlic) Tangawizi (ginger ) Binzari nyembamba (ground cumin 1/2 kijiko cha chai) Binzari manjano (turmeric 1/2 kijiko cha chai) Curry powder 1/2 kijiko cha chai Limao (lemon 1/2) Pilipili ya unga (chilli powder 1/2 kijiko cha chai) Giligilani (coriander kiasi) Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil) Unga wa ngano kiasi
Matayarisho
Katakata vitunguu na hoho katika vipande vidogo vidogo na kisha kwangua carrot na uweke pembeni. Chemsha viazi na chumvi kidogo vikiiva viponde na uviweke pembeni, Baada ya hapo tia nyama limao, chumvi, kitunguu swaum na tangawizi ichemshe mpaka iive na uhakikishe maji yote yamekauka. Kisha Tia binzari zote, pilipili, curry powder, giligilani, vitunguu, hoho na carrot. Pika mchanganyiko huo kwa muda wa dakika 3 na kisha ipua. Baada ya hapo changanya na viazi kisha tengeneza maduara ya kiasi na uyaweke pembeni. Chukua unga wa ngano kiasi na uchanganye na maji kupata uji usiokuwa mzito au mwepesi sana. baada ya hapo chovya madonge katika huo uji na uyachome katika mafuta. Hakikisha zinaiva na kuwa rangi ya brown na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.Unaweza ukazisevu na chatney yoyote unayopendelea.
Updated at: 2024-05-25 09:52:20 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa mchele ( Vikombe 2 vikubwa) Sukari (Nusu ya kikombe kikubwa) Hamira ( Nusu ya kijiko cha chai) Hiliki (Nusu ya kijiko cha chai) Tui la nazi ( Kikombe kimoja kikubwa) Unga wa ngano (Vijiko viwili vya chakula) Mafuta ya kuchomea (Vegetable oil)
Matayarisho
Unachanga unga, sukari, hamira, hiliki, unga wa ngano na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastiki. Kisha unaukoroga mpaka mchanganyiko unakuwa kama uji mzito. Kava bakuli lililokuwa na mchanganyiko kisha hifadhi katika sehemu yenye joto kwa muda wa masaa matatu.
Jinsi ya kupika
Weka chuma cha kuchomea vitumbua katika moto wa wastani, kisha weka mafuta kwenye chuma cha kuchomea ( Kijiko kimoja cha chai) mafuta yakisha pata moto tia uji wako (upawa mmoja) katika kila shimo la chuma cha kuchomea. Acha mpaka kitumbua kikauke kisha geuza na tia mafuta. Acha upande wa pili wa kitumbua mpaka uwe rangi ya kahawia na hapo kitumbua kitakuwa kimeiva utakitoa. Rudia hatua hizo kwa vitumbua vyote vilivyobaki.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 1 Kikombe
Sukari ya kusaga - 3/4 Kikombe
Siagi - 125 gms
Yai - 1
Baking powder - 1/2 kijiko cha chai
Zabibu kavu - 1/2 kikombe
Cornflakes iliyovunjwa (crushed) - 2 Vikombe
Vanilla - 1 kijiko cha chai
MAANDALIZI
Tia kwenye mashine ya kusaga (blender) au mashine ya keki, siagi, yai na vanilla uchanganye hadi ichanganyike vizuri. Tia baking powder, zabibu na unga na changanya vizuri. Paka siagi sinia ya kupikia ya oveni. Tengeneza viduara vidogo vidogo. Weka cornflakes katika sahani ya chali (flat) na zungusha viduara humo kisha upange katika sinia ya oveni. Pika katika moto wa 350ΒΊF kwa muda wa dakika 20-25 hadi vigeuke rangi na viwive.