Ni lazima asadiki kwamba;
- Mungu yupo mmoja. Bwana wetu na Baba yetu, mwenye kuwatunza watu wema mbinguni na kuwaadhibu watu wabaya motoni milele (Mt. 15:41,46)
- Katika Mungu mmoja kuna nafsi tatu: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Yoh. 14:16, 17).
- Nafsi ya pili alishuka duniani akajifanya mtu, akatuokoa utumwani mwa shetani, akatufundisha mambo gani tusadiki, mambo gani tutende, akatupa alama ya ukombozi wetu ndio ubatizo.
- Ubatizo wafuta kabisa uovu wa mtu na kutakasa roho zetu.
- Mwenye kubatizwa atubu na kurudisha alichoiba na kupatana na maadui n.k