Je, gongo na sigara husaidia uyeyushaji wa chakula?
ποΈ Ujana na Makuzi | Mapenzi na Ngono Salamaπ Kiswahili

Ni imani na fikra potofu kwamba, ukinywa gongo au kuvuta
sigara kwa kiasi kidogo baada ya chakula itasaidia kuyeyusha
baadhi ya vyakula vya mafuta. Pombe inaweza hata kupunguza
mtiririko wa kawaida wa kimiminika muhimu kwa uyeyushaji wa
chakula (tindikali) na hivyo kuchelewesha kuliko kurahisisha
uyeyushaji wa chakula.
Nikotini ya sigara kwa upande mwingine inaongeza kazi katika
utumbo mpana na hivyo kurahisisha uyeyushaji wa chakula.
Lakini kwa upande mwingine nikotini huchochea utengenezaji
wa tindikali tumboni ambayo husababisha maumivu ya tumbo.
β
Direct PDF download
The download button now generates the PDF on the server. It no longer depends on an off-screen browser canvas, so the former blank-PDF capture path is bypassed.