Processing Articles & Learning actionSaving securely and refreshing your workspace.
Je, sigara ni sumu kwa binadamu?
By SW - Melkisedeck Shine |
April 15, 2022
Ndiyo. Nikotini iliyo kwenye tumbaku ni sumu. Ukiwa na kiwango
kikubwa cha nikotini katika damu utajisikia kichefuchefu,
kutapika, kujaa kwa mate mdomoni, maumivu ya sehemu za
chini ya tumbo, kuharisha, na kujihisi dhaifu. Dalili nyingine
ni kuumwa na kichwa, kizunguzungu, kuongezeka kwa mapigo
ya moyo, kupata shinikizo la damu, kutetemeka na kutokwa na
jasho baridi. Nikotini nyingi inaweza kusababisha ukosefu wa
umakini na pia ukosefu wa usingizi.