VIAMBAUPISHI VYA TUNA

Tuna (samaki/jodari) - 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) - 4

Nyanya zilizosagwa - 5

Nyanya kopo - 3 Vijiko vya supu

Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo - cubes) - 4

Dengu (chick peas) - 1 kikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu

Hiliki - 1/4 kijiko cha chai

Mchanganyiko wa bizari - 1 kijiko cha supu

Chumvi - kiasi

Pilipili manga - 1 Kijiko cha chai

Vipande cha Maggi (Cube) - 2

VIAMBAUPISHI VYA WALI

Mchele - 3 Vikombe vikubwa (Mugs)

Mdalasini - 2 Vijiti

Karafuu - chembe 5

Zaafarani - kiasi
Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) - 1/2 Kikombe

JINSI YA KUANDAA

Kosha Mchele na roweka.
Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando.
Kaanga viazi, epua
Punguza mafuta, kaanga nyanya.
Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi.
Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi.
Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali.
Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu.
Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven)
Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali.
Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu).
Funika wali na upike katika jiko moto wa 450º kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.