MAHITAJI YA WALI

Mchele - 3 Magi

Mafuta - 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu - 3

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa - 1 kikubwa

Pilipli manga - 1/2 kijicho chai

Hiliki - 1/2 kijiko chai

Karafuu ya unga - 1/4 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga - 1/2 kijiko cha chai

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji - 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) - 1/4 kikombe

Chumvi kiasi

KUPIKA WALI

Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.
Tia vitunguu kisha tia bizari zote.
Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi
Tia mchele upike uwive.
Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.
Funika endelea kuupika hadi uwive.

MAHITAJI KWA NYAMA

Nyama - 2 Ratili (LB)

Chumvi - Kiasi

Mafuta - 1/4 kikombe

Kitunguu (kata virefu virefu) - 1 Kikubwa

Pilipili mboga kubwa - 2 ukipenda moja nyekundu moja kijani unazikata vipande virefu virefu.

Figili mwitu (celery) kata vipande virefu virefu- Miche miwili.

KUPIKA NYAMA

Chemsha nyama hadi iwive
Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu
Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu
Kaanga kidogo tu kama dakika moja.
Tayari kuliwa na wali.