ACKYSHINE ARTICLE Β· PRINTABLE READER

Jinsi ya kutengeneza Fagi Ya Kumumunyuka Mdomoni

✍️ SW - Melkisedeck ShineπŸ“… July 20, 2022πŸ’¬ 0 comments
πŸ—‚οΈ Dondoo za Mapishi na LisheπŸ—‚οΈ Upishi na Maandalizi ya Milo yenye Afya#Karibu AckySHINE🌐 Kiswahili
Jinsi ya kutengeneza Fagi Ya Kumumunyuka Mdomoni

VIAMBAUPISHI

Maziwa mazito matamu (condensed milk) - 2 vibati

Sukari - 1 kikombe

Samli 1 Β½ kikombe

Vanilla 2 kifuniko cha chupa yake

Hiliki ilosagwa - 2 vijiko vya chai

Sinia kubwa ya bati Paka samli

MAANDALIZI

Changanya maziwa, sukari na samli katika sufuria isiyogandisha chakula (non-stick) uweke katika moto.
Koroga huku ikipikika hadi ianze kugeuka rangi na kuanza kuachana. Usiache mkono kuroga isije kufanya madonge.
Tia hiliki na vanilla, endelea kuipika.
Itakapogeuka rangi vizuri mimina katika sinia na haraka uitandaze kwa mwiko huku ukiuchovya katika maji na kuendelea kuitandaza hadi ikae sawa kote.
Pitisha kisu kuikataka ili ikipoa iwe wepesi kuitoa vipande.

Kila inapozidi kupoa na kukaa ndipo fagi inakauka na kumumunyuka.

βœ…
Direct PDF download

The download button now generates the PDF on the server. It no longer depends on an off-screen browser canvas, so the former blank-PDF capture path is bypassed.