Viamba upishi

Unga 4 Vikombe vya chai Sukari ya laini (icing sugar) 1 Kikombe cha chai Baking powder 2 Vijiko vya chai Mayai 2 Siagi au margarine 1 Kikombe cha chai Vanilla 1 Kijiko cha chai Maziwa ya kuchanganyia kiasi Tende iliyotolewa koko 1 Kikombe ufuta (sasame) kiasi 1/4 kikombe Jinsi ya kuandaa na kupika 1. Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika mashine. 2. Kisha tia mayai, vanilla na halafu maziwa kidogo kidogo hadi mchanganyiko ushikamane. 3. Gawanya madonge mawili na usukume kama chapati, lakini sio nyembamba sana. 4. Tandaza tende robo ya duara na unyunyize ufuta duara zima: kisha kunja hadi mwisho na ukate kate, kisha upange katika trei ya kuvumbika. 5. Vumbika (bake) moto wa 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi vigeuke rangi na viwive. 6. Zikisha iiva ziache zipowe na zitakuwa tayari kuliwa.