πKuweka nia njema
<p>Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.</p>
Open printable article βπSala ya Malaika wa Bwana
<p>Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,β¦.</p><p>Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, β¦β¦<br />Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, β¦..</p><p>Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.</p>
Open printable article βπSala kwa Mtakatifu Yosefu
<p>Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda nayo Bikira Mtakatifu, Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya tunza ya Baba, uliyomtunza nayo Mtoto Yesu, tunakuomba sana, utuangalie kwa wema, sisi tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tuliokombolewa kwa damu yake, utusimamie katika masumbuko yetu, kwa enzi na shime yako.<br /><br /></p>
Open printable article βπSALA YA KUOMBEA FAMILIA
<p>Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.</p>
Open printable article βπSala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua
<p>Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaokusihi, tufurahie hali njema ya hewa na mvua tunayoitamani na kuhitaji. Tutumie daima vipawa vya wema wako kwa ajili ya utukufu wa jina lako, na kwa ajili ya wokovu watu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana</p>
Open printable article βπSala ya Usiku kabla ya kulala
<p>Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.</p><h2>SALA YA KUSHUKURU</h2><p>Tunakushukuru, ee Mungu, kwa mapaji uliyotujalia leo. Amina.</p><p>Baba yetu β¦</p><p>Salamu Maria β¦</p>
Open printable article βπSALA YA MAPENDO
<p>Mungu wangu, nakupenda zaidi ya cho chote, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina</p>
Open printable article βπAMRI ZA MUNGU
<p>1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE.<br />2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO.<br />3. SHIKA KITAKATIFU SIKU YA MUNGU.<br />4. WAHESHIMU BABA NA MAMA, UPATE MIAKA MINGI NA HERI DUNIANI.</p>
Open printable article βπSala ya Asubuhi ya kila siku
<p>Kwa jina la Babaβ¦..</p><p>Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu.<br />Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho.<br />Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.Naomba sana Baba wee, baraka yako nipokee.<br />Bikira safi, Ee Maria nisipotee nisimamie.<br />Mlinzi mkuu malaika wee kwa Mungu wetu niombee,nitake nitende mema tu na mwisho nije kwako juu.Amina.</p>
Open printable article βπMalkia wa Mbingu
<p>Malkia wa mbingu, furahi, aleluya. Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya. Amefufuka alivyosema, Aleluya. Utuombee kwa Mungu, Aleluya. Furahi shangilia, ee Bikira Maria, Alaluya. Kwani hakika Bwana amefufuka Aleluya.Β </p>
Open printable article βπNovena ya Noeli
<p>Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)</p><p>Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku wa Noeli, tar 24 Disemba. Inajulikana kama novena ya Mt. Andrea kwa sababu novena hii huanza kusaliwa katika siku ya kumbukumbu ya Mt. Andrea Mtume.</p>
Open printable article βπSala ya Saa Tisa
<p>βββ</p><p>Sala ya saa tisaππΎ</p><p>Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. A mina</p><p>Yesu, ulikufa, lakini chanzo cha uhai kilitoka kwa ajili ya watu, na bahari ya huruma ilifunguka kwa ajili ya ulimwengu mzima. Ee chemchemi ya Uhai, huruma ya Mungu isiyo na mwisho, ikafunika ulimwengu mzima na ukajimwaga mwenyewe juu yetu.</p>
Open printable article βπSALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI
<p>Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Maria Bikira Milele, na mkubwa wa Familia Takatifu. Umechaguliwa na Mwakilishi wa Kristu kama Msimamizi wa kimbingu na mlinzi wa Kanisa alilolianzisha Kristu. Ndiyo maana ninakuomba kwa matumaini makuu usaidizi wako wenye nguvu kwa ajili ya Kanisa zima duniani.</p>
Open printable article βπLitani ya Bikira Maria
<p>Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.</p>
Open printable article βπSALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA
<p><em>Sala hii ilipatikana katika mwaka wa hamsini wa Bwana na Mwokozi Wetu Yesu Kristu. Mnamo mwaka 1505 Baba Mtakatifu alimtumia sala hii Mfalme Charles wakati alipokuwa anaenda vitani. Yeyote atakayeisoma sala hii, au kuisikia ikisomwa, au kuibeba, hatakufa kifo cha ghafla,hatazama majini, hatadhurika kwa sumu, wala hataanguka katika mikono ya adui zake, au kuunguzwa katika moto wowote ule, au kushindwa katika vita.</em></p>
Open printable article β