πSALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO
<p>ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA</p><p>Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.</p><p>TESO LA KWANZA</p><p>Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.<br />Tuombe neema ya kuvumilia mateso.<br />Mama wa mateso utuombee.</p>
Open printable article βπROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU
<p><strong>Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.</strong></p><h2>Kwenye Msalaba Sali:</h2><p>βEe Yesu tupe moyo wako kama amana ya upendo wako na kimbilio letu, ili tupate pumziko salama wakati wa maisha yetu na faraja tamu saa ya kufa kwetuβ.<br />Baba Yetu β¦β¦..<br />Salamu Maria β¦β¦. (mara tatu)<br />Nasadiki β¦β¦β¦..</p>
Open printable article βπSala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu
<p>Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.</p>
Open printable article βπNOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU
<p>Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu,; anza Novena kwa Moyo Mtk wa Yesu katika Alhamisi ya Sikukuu ya Ekaristi Takatifu (Corpus Christi), yaani Alhamisi ya wiki moja kabla ya Sikukuu ya Moyo Mtk (au Alhamisi baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk). Endapo Sikukuu hii itaadhimishwa siku ya Dominika inayofuata Sikukuu yenyewe kama inavyofanyika mahali pengi, basi novena inatakiwa ianze Ijumaa ya baada ya Sikukuu ya Utatu Mtk ili imalizike Jumamosi kabla ya Dominika ya sikukuu hii ya Moyo Mtk kwa Yesu.</p>
Open printable article βπSALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI
<p>Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,<br />Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,<br />Uwe nami leo hii,<br />Kuniangaza na kunilinda,<br />Kunitawala na kuniongoza.<br />Amina.</p>
Open printable article βπLITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO
<p>Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie<br />Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie<br />Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie<br />Kristo utusikie β Kristo utusikilize<br />Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie<br />Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie<br />Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie</p>
Open printable article βπSALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU
<p>Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.</p>
Open printable article βπSALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU
<p>Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.Β <strong>Amina.</strong></p>
Open printable article βπSALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU
<p>Baba yetu uliye mbinguni<br />Jina lako litukuzwe<br />Ufalme wako ufike<br />Utakalo lifanyike<br />Duniani kama mbinguni<br />Utupe leo mkate wetu wa kila siku<br />Utusamehe makosa yetu<br />Kama tunavyowasamehe<br />Na sisi waliotukosea<br />Usitutie katika kishawishi<br />Lakini utuopoe maovuni.<br />Amina.</p>
Open printable article βπSALA ZA KUMWABUDU YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU
<p>Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti Takatifu ya Altare;/ pokea kitendo hiki cha kukuangukia kifudi fudi/ kama ishara ya tamaa niliyonayo ya kukuabudu Wewe/ bila kuchoka/ na kukushukuru kwa mapendo yako makubwa/ yasiyo na kipimo/ ambayo Moyo wako Mtakatifu sana/ unawaka katika Sakramenti Takatifu hii.</p>
Open printable article βπSALA YA MTU ALIYEKABILIWA NA MATATIZO MBALIMBALI
<p>Ewe Mtakatifu Yuda Tadei,/ mtume mtukufu na shahidi wa Kristo,/ umesifika pote kwa wepesi wako wa kutoa misaada/ kwa wanaokukimbilia katika matatizo yao mazito./ Pia ni mwombezi wa waliopondeka moyo./</p><p>Β </p>
Open printable article βπSALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I
<p>Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate wa kidunia/ ukafanya mwujiza na kuugeuza/ kuwa Mwili wako azizi./ Kwa mapendo ukawapa Mitume Mwili huo/ uwe kumbukumbu la mateso yako mastahivu./ Uliwaosha miguu kwa Mikono yako Mitakatifu.</p>
Open printable article βπSALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA
<p>Kwa njia ya Maji haya ya Baraka, na kwa njia ya Damu yako azizi, na kwa maombezi ya Moyo Safi wa Maria, unioshe na uovu wangu wote na uwasaidie roho zinazoteseka toharani. Amina.</p>
Open printable article βπAMRI ZA KANISA
<p>1. HUDHURIA MISA TAKATIFU DOMINIKA NA SIKUKUU ZILZOAMRIWA</p><p>2. FUNGA SIKU YA JUMATANO YA MAJIVU; USILE NYAMA SIKU YA IJUMAA KUU</p><p>3. UNGAMA DHAMBI ZAKO WALAU MARA MOJA KILA MWAKA</p>
Open printable article βπSALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI
<p>Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkingaji na mteteaji wangu. Naweka roho fukara katika moyo wako uliotobolewa na panga nyingi za mateso. Unipokee mimi niwe mtumishi wako wa pekee na mshiriki wa mateso yako. Nijalie nguvu niwe daima karibu na msalaba ule alikosulibiwa Yesu. Nakutolea nafsi yangu na mali yangu yote.Β </p>
Open printable article β